Kitomo
Kitomo kahawia (Zebrasoma scopas)
Kitomo kahawia (Zebrasoma scopas)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Actinopterygii (Samaki walio na mapezi yenye tindi)
Oda: Perciformes (Samaki kama ngege)
Familia: Acanthuridae (Samaki walio na nasaba na kangaja)
Bonaparte, 1832
Jenasi: Jenasi 2:
Spishi: Spishi 8:

Vitomo, vyelwende, vitatange, vitogoo au vitubaku ni samaki wa baharini wa jenasi Paracanthurus na Zebrasoma katika familia Acanthuridae wa oda Perciformes ambao wanafanana na kangaja lakini wana pezimgongo na pezimkundu makubwa kama tanga.

Maelezo hariri

Kama kangaja vitomo wana miiba kwa umbo la vijembe, mmoja kwa kila upande wa msingi wa mkia ("mikia ya miiba"), ambayo ni mikali na hatari sana. Kwa sababu hii, samaki hawa pia wana rangi kali za onyo. Pezimgongo na pezimkundu ni makubwa, katika jenasi Zebrasoma hasa, na yanafanana na tanga. Mdomo mdogo una safu moja ya meno yanayotumika kwa kujilisha na miani. Mdomo wa spishi za Zebrasoma unatokeza sana.

Spishi hariri

Picha hariri

Marejeo hariri

  • Rashid Anam & Edoardo Mostarda (2012) Field identification guide for the living marine resources of Kenya. FAO, Rome.
  • Gabriella Bianchi (1985) Field guide to the commercial marine brackish-water species of Tanzania. FAO, Rome.

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mnyama fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kitomo kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.