Kiunguja ("lugha ya Unguja") ni lahaja ya Kiswahili iliyo lugha ya kawaida kwenye kisiwa cha Unguja, Zanzibar, Tanzania.

Lahaja hiyo ilitumiwa wakati wa ukoloni na Kamati ya kimaeneo ya lugha ya Kiswahili kama msingi wa kuunda Kiswahili Sanifu katika Afrika ya Mashariki [1] kutokana na sababu zifuatazo:

  1. Kiunguja mjini ni lahaja iliyopata kuenea sehemu kubwa sana, kwani kilipata kuenea kutoka Unguja mjini, Zanzibar kwa ujumla, Tanganyika na hata Mombasa - Kenya.
  2. Ni lahaja iliyokuwa na watumiaji wengi, kutokana na ile kasi yake kubwa ya kuenea kutoka Zanzibar hadi nchi jirani.
  3. Ni lahaja ilitokuwa na msamiati na utamkaji mwepesi ukilinganisha na lahaja nyingine za kiswahili.
  4. Pia Kiunguja mjini kilipata kufanyiwa tafiti nyingi hata kabla ya kusanifishwa kwake. Jambo hili lilipelekea lahaja hiyo kuwa na machapisho mengi.

Marejeo hariri