Flag of Tanzania
Flag of Tanzania
Coat of Arms of Tanzania
Coat of Arms of Tanzania
Location on the world map

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi ya kati katika Afrika ya Mashariki, imepakana na Kenya na Uganda kwa upande wa kaskazini, Rwanda, Burundi na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwa upande wa magharibi, na Zambia, Malawi na Msumbiji zipo upande wa kusini. Hii ni moja kati ya nchi zilizopo upande wa mashariki mwa Bahari ya Hindi.

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni jamhuri iliyounganisha mikoa 26 ya nchi. Rais wa nchi wa sasa ni Mh. Jakaya Mrisho Kikwete, alichaguliwa mnamo mwaka wa 2005. Tangu 1996, mji mkuu wa Tanzania ulikuwa Dodoma, ambamo makao makuu ya serikali ndipo yalipo. Baada ya kuwa huru mnamo 1996 mji mkubwa wa pwani ya Dar es Salaam ukawa mji mkuu wa kisiasa. Leo hii jiji la Dar es Salaam limebaki kuwa kama jiji la kibiashara katika Tanzania, na ndiyo bandari kubwa ya nchi na pia majirani zake hutumia bandari hii.

Jina la Tanzania ni muunganiko baina ya Tanganyika na Zanzibar, nchi hizi mbili ziliungana mnamo 1964 na kuunda Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, ambazo baadaye katika mwaka huohuo jina likabadilishwa na kuwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.