Lynne Muthoni Wanyeki

Mwanaharakati wa Haki za Binadamu

Lynne Muthoni Wanyeki (alizaliwa 1972) ni mwanasayansi, mwanaharakati wa haki za binadamu, mwandishi wa habari wa Kenya. Ndiye Mkurugenzi wa sasa wa kanda wa Ofisi ya Kanda ya Afrika ya Open Society Foundation. Wanyeki ni Mkurugenzi wa Kanda wa zamani wa Ofisi ya Kanda ya Amnesty International kwa Afrika Mashariki, Pembe ya Afrika, na Maziwa Makuu.[1] Yeye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa zamani wa Tume ya Haki za Binadamu ya Kenya na Mtandao wa Maendeleo ya Wanawake na Mawasiliano wa Afrika.[2]

Maisha ya awali na elimu

hariri

Wanyeki alizaliwa na mama mwenye asili ya Kanada na baba Mkenya, kabila la Kikuyu, na alikulia nchini Kenya. Baba yake alikufa mnamo 1991.

Ana shahada ya sanaa katika Sayansi ya Siasa (mahusiano ya kimataifa) na Kifaransa (fasihi) kutoka Chuo Kikuu cha New Brunswick na Chuo Kikuu cha Simon Fraser mtawalia.[3] Wanyeki pia ana shahada ya uzamili katika masuala ya utawala wa umma kutoka L'Institut d'études politiques huko Paris na kwa sasa anaendeleza masomo yake ya udaktari katika Idara ya Siasa na Mafunzo ya Kimataifa katika Shule ya School of Oriental and African Studies (SOAS).[4]

Wanyeki alianza kazi yake kama mwanaharakati aliyelenga haki za wanawake mwaka wa 1988, alipokuwa akisomea shahada yake ya kwanza nchini Kanada. Nchini Kanada pia alianza katika vyombo vya habari, akifanya kazi na magazeti ya ndani na vituo vya redio kuhusu masuala yanayohusiana na wahamiaji na wanawake wakimbizi.[5]

Aliporejea Kenya baada ya chuo kikuu, mojawapo ya kazi za kwanza za Wanyeki zilihusisha kazi ya maendeleo katika maeneo ya Ukambani, ambako alifanya kazi ya kujitolea katika shirika la Oxfam na Mpango wa Mazingira wa Umoja wa Mataifa.[6] Mwishoni mwa miaka ya 1990, alifanya kazi Nairobi kama wakala wa shirika la habari la uteteziInter Press Services la nchini Italia. Akiwa na umri wa miaka thelathini alichukua nafasi ya Njoki Wainaina kama mkurugenzi mkuu wa Mtandao wa Maendeleo ya Wanawake wa Afrika na Mawasiliano yaani African Women's Development and Communication Network(FEMNET),. Mwanzoni, aliliona shirika hilo kuwa lenye kutawaliwa na baraza la wanawake wazee wenye msimamo mkali. Baadaye aligundua kuwa nafasi yake ilimpa uaminifu kama mzungumzaji anayetafutwa sana juu ya haki za binadamu, usawa wa kijinsia na maendeleo. Pia alianza kuandika makala ya kila wiki katika gazeti la Afrika Mashariki.[7]

Mnamo Machi 2018, Wanyeki alikuwa mmoja wa waandishi wanane waliojiondoa kwenye Nation Media Group wakipinga kile walichokiona kuwa uingiliaji mwingi wa serikali ya Kenya na ukiukaji wa uhuru wa vyombo vya habari.[8]

Marejeo

hariri
  1. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2023-07-25. Iliwekwa mnamo 2024-06-13.
  2. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhiwa kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2023-07-25. Iliwekwa mnamo 2024-06-13.
  3. https://web.archive.org/web/20171201041213/https://www.soas.ac.uk/staff/staff88629.php
  4. https://web.archive.org/web/20171201041213/https://www.soas.ac.uk/staff/staff88629.php
  5. https://nation.africa/lifestyle/1190-378512-fdf3rsz/index.html[dead link]
  6. https://magja.net/%20[L,R=301,NC[dead link]]
  7. https://books.google.co.tz/books?id=ikfru3xCQE8C&pg=PA45&redir_esc=y#v=onepage&q&f=false
  8. https://www.aljazeera.com/news/2018/3/27/key-nmg-staff-quit-for-lack-of-media-freedom