M-pesa ni huduma ya kutuma pesa kwa kutumia simu ya mkononi inayotolewa na kampuni ya Safaricom.

Nembo la M-Pesa

Kenya ndiyo nchi ya kwanza kutumia huduma hiyo maarufu ambayo ilizinduliwa mwezi Aprili mwaka wa 2007 kwa ushirikiano kati ya Safaricom na Vodafone. Tangu wakati huo, Mpesa imetia fora sana, hasa kwa wananchi wa mapato ya chini wasio na akaunti za benki. Kulingana na takwimu rasmi za Safaricom, M-pesa ina wateja zaidi ya milioni saba na imewezesha Wakenya kutuma na kupokea takriban shilingi bilioni 230 kufikia Agosti 2009. Mwaka huo, Safaricom iliboresha huduma hii hivi kwamba Wakenya wanaweza kupokea pesa moja kwa moja kutoka kwa jamaa zao walioko nchini Uingereza.

Baadhi ya mambo yanayoipa umaarufu huduma hii ni kama vile urahisi wa kuitumia na kwamba mtu hahitaji kuwa na akaunti ya benki kutuma au kupokea pesa. Isitoshe, usalama wake ni wa hali ya juu na anayeitumia hupokea ujumbe mfupi papo hapo kudhibitisha kuwa ametuma au kupokea kiasi fulani cha pesa kwa/kutoka mtu fulani. Kwa sasa, huduma hii imepanuliwa na kuwawezesha Wakenya kulipia bidhaa na huduma kadha wa kadha, kama vile stima, maji, posta, nauli, karo, na hata mishahara ya wafanyikazi.

Safaricom hariri

Kampuni ya Safaricom, ambayo ilisajiliwa katika Soko la Hisa la Nairobi inaongozwa na Michael Joseph, Afisa Mkuu Mtendaji ambaye amekuwa katika hatamu za uongozi wa kampuni hii yenye mgawo mkubwa zaidi wa wateja nchini Kenya tangu ilipoanzishwa mwaka wa 2000. Kuimarika kwake kumeifanya kutambulika kama Kampuni inayoheshimika zaidi katika Afrika Mashariki kwa miaka mitatu mfululizo.

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya uchumi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu M-pesa kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.