Mama ni mwanamke anayemlea mtoto hasa aliyemzaa mwenyewe, lakini pengine sivyo, lakini anamlea. Upande wa pili anatarajiwa kuwepo baba, yaani mwanamume aliyeshirikiana naye katika kuzaa au anashirikiana naye katika kulea.

Mama na mtoto wakifurahi pamoja.
Monumento a la Madre (yaani Mnara kwa heshima ya Mama) huko Mexico City. Maandishi yake yanasema: "Kwa yule aliyetupenda kabla hajakutana nasi".
Upendo ulivyochorwa na Mfaransa William-Adolphe Bouguereau.

Wale ambao si wazazi wanaitwa ka kawaida "mama wa kambo" na "baba wa kambo".

Katika historia na utamaduni wa makabila na mataifa mengi, umama ni sifa maalumu ya mwanamke inayotangaza kuwa amekomaa na kukamilika kwa kuendeleza uhai wa binadamu kadiri anavyoelekezwa na umbile lake upande wa mwili na wa nafsi.

Wastani wa idadi ya watoto wanaozaliwa na mwanamke mmoja unatofautiana sana: mwaka 2013 ule mkubwa zaidi ulipatikana Niger (7.03 watoto waliozaliwa na kila mwanamke) na ule ndogo zaidi Singapore (0.79 tu).[1]

Jina hilo au lingine la kufanana linatumika katika lugha nyingi duniani, kwa sababu "neno la kwanza" la mtoto ni "ma" au "mama".

Kwa Kiswahili neno "mama" pia hutumika kama neno la heshima kwa wanawake hasa wa umri mkubwa kiasi. Mara nyingi hutumiwa pia ndani ya familia na mume kumwita mke wake.

Tanbihi

  1. Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2009-10-28. Iliwekwa mnamo 2015-03-08.

Marejeo

Viungo vya nje

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu: