Mariam Salum Mfaki

Mwanasiasa wa Tanzania


Mariam Salum Mfaki alikuwa mwanasiasa wa Tanzania. Aliwahi kuwa Mbunge wa viti maalumu wa Bunge la Tanzania jijini Dodoma tangu mwaka 2000 mpaka alipofariki mwaka 2015.[1]

Mariam Salum Mfaki
Mbunge wa Viti Maalumu
Bunge la Tanzania
Jimbo la uchaguzi Kondoa
Tarehe ya kifo 2015
Chama Sauti ya Umma
Tar. ya kuingia bunge
Aliondoka 2015

Mfaki alianza kujihusisha na siasa akiwa katibu wa umoja wa wanawake wa Chama Cha Mapinduzi (CCM)(UWT) katika wilaya ya Kondoa, tangu mwaka 1973 mpaka 1976.[1] Baadae alichaguliwa kuwa katibu wa chama hicho cha wanawake kimkoa, hivyo alikuwa katibu wa umoja wa wanawake mkoa wa Dodoma tangu mwaka 1976 mpaka mwaka 1983[1]. Alipata uhamisho kwenda ofisi ya waziri mkuu kama katibu. Alitumikia nafasi ya ukatibu katika ofisi ya waziri mkuu tangu mwaka 1984 mpaka 1998.[1]

Kifo hariri

Mfaki alifariki katika hospitali ya Mkoa wa Dodoma akiwa na umri wa miaka 69[1]; alikuwa amegundulika akiwa na kansa mwaka 2012, alizikwa kijijini kwao mkoani Dodoma.[1]

Marejeo hariri

  1. 1.0 1.1 1.2 1.3 1.4 1.5 "Mariam Mfaki (MP) is dead", Daily News (Tanzania), 2015-07-22. Retrieved on 2015-08-19. Archived from the original on 2019-05-06. 
  Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mariam Salum Mfaki kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.