Mauro wa Parenzo (alifariki Porech, leo nchini Korasya, 305 hivi) alikuwa askofu wa kwanza wa mji huo.

Mt. Mauro (wa tatu kuanzia kushoto) akishika mikononi taji la wafiadini.

Inasemekana alitokea Afrika Kaskazini na kuwahi kuishi miaka kumi na nane monasterini. Hatimaye aliteswa sana akauawa kwa kukatwa kichwa katika dhuluma ya kaisari Dioklesyano[1].

Tangu kale anaheshimiwa na madhehebu mbalimbali ya Ukristo kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 21 Novemba[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.