Miikka Aleksanteri Kari (amezaliwa tar. 16 Oktoba 1971, mjini Helsinki, Ufini) ni mtayarishaji wa muziki na mhandisi wa sauti toka nchini Ufini-Tanzania. Anafahamika zaidi kwa jina lake la kitayarishaji kama Miikka Mwamba. Miikka Mwamba ni mtayarishaji mashuhuri sana kwa nchi ya Tanzania, na ameweza kujibebea umaarufu mkubwa sana nchini Tanzania kunako miaka ya 2000.

Miikka Mwamba
Miikka Mwamba.
Miikka Mwamba.
Maelezo ya awali
Jina la kuzaliwa Miikka Aleksanteri Kari
Amezaliwa 16 Oktoba 1971 (1971-10-16) (umri 52)
Asili yake Finland
Aina ya muziki Hip hip
R&B
Dansi
Pop
Kazi yake Mtayarishaji
Studio Mwamba Productions
FM Studio
Kokwa Records
Tovuti Mwambaproductions.com

Miikka aliwahi kufanya kazi na wasanii mbalimbali wa nchini Tanzania. Wasanii hao ni: Dully Sykes, Inspector Haroun, Lady Jay Dee, Mad Ice, Chegge, Mandojo na Domo Kaya, Solid Ground Family, Complex, Zahrani (maarufu kama Big Punisher wa Bongo), Only Face, Dknob na wengine wengi wa kutoka Tanzania.

Miikka Mwamba, ameshawahi kufanya kazi miaka mingi kwenye medani za muziki, filamu, michezo ya kuigiza na dansi, ni swala ambalo si mara nyingi kufanyika kwa nchi ya Ufini na Tanzania pia.

Miikka alihitimu elimu yake ya msingi na secondary katika Lohja, ambacho ni chuo cha sanaa (Torkkelin kuvataidelukio) alisomea Helsinki, na shahada ya uzamili (MA) alipata Theatre Academy of Finland, Dept. of Light and Sound Design.

Nyimbo zilizotamba hariri

  • Julieta - Dully Sykes (2000)
  • Athumani Mlevi - Solid Ground Family (2001)
  • Baby Gal - Mad Ice (2002)
  • Tupa Mawe - Zahrani na Complex (2001)
  • Twenzetu - Chegge, Ferouz na Mh Temba (2005)
  • Elimu Mitaani.com - Dknob (2003)
  • Kitu Gani - Dknob (2007)

Viungo vya Nje hariri