Mto Berg (pia unaitwa Berg River, Great Berg River au kwa Kiafrikaans: Bergrivier) ni mto uliopo kaskazini mwa Cape Town ndani ya jimbo la Rasi ya Magharibi ya Afrika Kusini na unatiririka kwenda Bahari ya Atlantiki.

Lambo la Mto Berg linahifadhi maji kwa matumizi ya Cape Town

Mto una takriban km 294 kwa urefu na beseni lenye ukubwa wa km² 7,715.

Takribani % 65 za eneo la Mto Berg linatumika kwa kilimo.

Miji mikubwa katika eneo la Mto Berg ni Velddrif na Laaiplek karibu na ukanda wa pwani, Piketberg, Hopefield, Moorreesburg na Darling kwa ukanda wa ndani  wa ardhi.

Tazama pia hariri

  Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika Kusini bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Mto Berg kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.