Kiafrikana

Lugha ya Kijerumani Magharibi, inayozungumzwa nchini Afrika Kusini na Namibia
(Elekezwa kutoka Kiafrikaans)

Kiafrikana[1] au Kiafrikaans ni lugha ya Afrika Kusini iliyotokea katika karne nne zilizopita kwenye msingi wa Kiholanzi pamoja na athari za lugha mbalimbali. Hata kama ni lugha iliyozaliwa Afrika na kujadiliwa hapa, kitaalamu ni kati ya lugha za Kijerumaniki.

Kiafrikana
Afrikaans (af)
Lugha
Asili Afrika Kusini
Namibia
Botswana
Zimbabwe
Wasemaji

L1 : 7.2 Milioni
L2: 10 Milioni

Jumla: 17.2 Milioni
Familia za lugha Kihindi Kiulaya
Kijerumaniki
Kijerumaniki cha Magharibi
Kiholanzi
Aina za Awali Kiholanzi cha Kati
Kiholanzi cha Kaskazini
Kiafrikana cha Kale
Mfumo wa kuandika Kilatini
Lugha Rasmi
Lugha rasmi kwa Afrika Kusini
Namibia
Nambari za Msimbo
ISO 639-1 af
ISO 639-2 afr
Glottolog afri1274

Wasemaji wa Kiafrikana

Imekuwa lugha rasmi katika Afrika Kusini tangu mwaka 1925 badala ya Kiholanzi. Hadi sasa ni lugha rasmi mojawapo Afrika Kusini pamoja na lugha 9 nyingine. Ni pia kati ya lugha za taifa huko Namibia.

Colins kutoka Cape Town anaongea Kiafrikana.

Kiafrikana kina wasemaji wa lugha ya kwanza milioni saba ambao ni sawa na 13.5% za raia wa Afrika Kusini, ambako ni lugha ya tatu wenye wasemaji wengi baada ya Kizulu na Kixhosa.[2] Wasemaji wote hukadiriwa kuwa kati ya milioni 15 hadi 23.

Ni lugha kuu kwenye nusu ya magharibi ya Afrika Kusini yaani kwnye majimbo ya Rasi ya Kaskazini na Rasi ya Magharibi. Kufuatana na sensa ya 2011 wasemaji wa Kiafrikana ni Machotara wa Afrika Kusini milioni 4.8, Wazungu wa Afrika Kusini milioni 2.7, Waafrika Weusi 600,000 na Wahindi wa Afrika Kusini 58,000.

Kiasili kilianzisha kutokana na Kiholanzi cha makaburu wa kwanza kikapokea asilimia 5-10 za msamiati kutoka lugha za Khoikhoi, Wareno, Wabantu, Wajerumani, Wafaransa na Waingereza. ya Afrika Kusini lakini imekuwa pia lugha ya wakazi chotara katika jimbo la Rasi Magharibi ("Cape Coloureds"). Leo hii wasemaji wa asili ya Ulaya ni chini ya nusu ya wasemaji wote wa Kiafrikana.

Inatumika pia Botswana, Eswatini na Zimbabwe.

Marejeo

  1. TUKI. Kamusi ya Kiswahili Sanifu (tol. la 4). uk. 237.
  2. Census 2011: Census in brief (PDF). Pretoria: Statistics South Africa. 2012. uk. 27. ISBN 9780621413885. Ilihifadhiwa kwenye nyaraka (PDF) kutoka chanzo mnamo 13 Mei 2015.

Viungo vya nje

  Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kiafrikana kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.