Njozi ni istilahi inayotumika hasa katika maisha ya kiroho kama njia ya mtu kupata taarifa ya mambo yaliyopita, yaliyopo, na yale yajayo.

Neno hilo hutumiwa pia kwa maana ya ndoto, ambayo ni ya kawaida pale mtu anapokuwa amepumzisha akili na mwili.

Upande wa dini huaminiwa kuwa Mungu hutumia njozi kuwasilisha ujumbe kwa mtu, kama habari juu ya kazi yake au tukio linalotaka kutukia. Kwa kifupi tu Njozi ni tukio lolote la ndoto inaweza kuwa nzuri au mbaya

Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.