Patrolojia (kwa Kiingereza "Patrology", kutokana na maneno ya Kigiriki "pater", baba na "logia", elimu) ni taaluma inayohusu mafundisho ya mababu wa Kanisa (karne ya 1 hadi ya 8).

Muhimu zaidi upande wa Mashariki ni: Atanasi, Basili Mkuu, Gregori wa Nazienzi na Yohane Krisostomo.

Upande wa Magharibi ni: Ambrosi, Agostino wa Hippo, Jeromu na Papa Gregori I.

Umuhimu wa fani hiyo unatokana na kwamba watu hao waliishi jirani kidogo na wakati ambapo Yesu na mitume wake waliishi duniani, hivyo waliweza kujua na kuelewa zaidi mafundisho yao, ambayo ndiyo utimilifu wa ufunuo wa Mungu kadiri ya Ukristo.

Kwa msingi huo, Wakatoliki, Waorthodoksi na Waorthodoksi wa Mashariki wanazingatia sana maandishi yao, hasa yanapolingana ingawa yalitolewa katika mazingira mbalimbali, kama uthibitisho wa uwepo wa mapokeo ya Mitume.

Maandishi yao mengi ni kwa lugha ya Kigiriki na ya Kilatini, lakini yapo pia ya Kiaramu, Kimisri, ya Kigeez, ya Kiarmenia n.k.

Kwa kiasi kikubwa yalikusanywa na padri Jacques Paul Migne katika magombo mengi ya:

Hata hivyo wataalamu wanazidi kuyatoa upya kwa usahihi zaidi na kutoa mengine yaliyopatikana baada ya toleo la Migne.

Vyanzo na viungo vya nje hariri

Kwa sauti
  Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Patrolojia kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.