Sagita (kundinyota)
.
Sagita (kwa Kilatini na Kiingereza Sagitta) [1] ni jina la kundinyota ndogo iliyopo kwenye nusutufe ya kaskazini ya Dunia.
Mahali pakeEdit
Sagita (Sagitta) lipo karibu na nyota angavu za Vega na Tairi. Inapakana na makundinyota jirani ya Mbweha (Vulpecula), Rakisi (Hercules), Ukabu (Aquila) na Dalufnin (Delphinus)'.
JinaEdit
Sagita (Sagitta) lilijulikana kwa mabaharia Waswahili tangu miaka mingi wakifuata njia yao baharini wakati wa usiku kwa msaada wa nyota. Walipokea jina hili kutoka kwa Waarabu wanaosema السهم as-sahm kwa maana ya “mshale” [2]. Waarabu walitafsiri hapa jina la Ptolemaio aliyetaja nyota hizi vile kwa jina la Βέλος Velos katika orodha yake ya Almagesti.
Sagitta - Sagita ni kati ya makundinyota 48 yaliyotajwa tayari na Klaudio Ptolemaio katika kitabu cha Almagesti wakati wa karne ya 2 BK. Lipo pia katika orodha ya makundinyota 88 yaliyorodheshwa na Umoja wa Kimataifa wa Astronomia [3] kwa jina la Sagitta. Kifupi chake rasmi kufuatana na UKIA ni 'Sge'.[4]
NyotaEdit
Nyota angavu zaidi ni Gamma Sagittae. Ina mwangaza unaoonekana wa mag 3.5 ikiwa na umbali wake unakadiriwa kati ya miakanuru 258 kutoka Dunia[5][6].
Jina la (Bayer) |
Namba ya Flamsteed |
Jina (Ukia) |
Mwangaza unaoonekana |
Umbali (miakanuru) |
Aina ya spektra | |||||
---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|---|
γ | 12 | 3,5m | M0 III | |||||||
δ | 7 | 3,7m | M2 II + B6 | |||||||
β | 6 | 4,4m | G8 IIIa | |||||||
α | 5 | Sham | 4,4m | - |
TanbihiEdit
- ↑ Uhusika milikishi (en:genitive) ya "Sagitta" katika lugha ya Kilatini ni "Sagittae" na hili ni umbo la jina linaloonekana katika majina ya nyota za kundi hili kama vile Alfa Sagittae, nk.
- ↑ ling. Knappert 1993; anarejelea jina la Kiarabu kuwa "Sahm al Hamsa" yaani "mishale mitano"
- ↑ The Constellations, tovuti ya International Astronomical Union , iliangaliwa Julai 2017
- ↑ Russell, Henry Norris (1922). "The New International Symbols for the Constellations". Popular Astronomy 30: 469–71.
- ↑ Sagitta, tovuti ya Constellation Guide, iliangaliwa Oktoba 2017
- ↑ Gammaa Sagittae, tovuti ya Prof. Jim Kaler
Viungo vya NjeEdit
- Constellation Guide: Sagitta constellation
- Sagitta, "Stars", kwenye tovuti ya Prof Jim Kaler, University of Illinois, iliangaliwa Oktoba 2017
- Star Tales – Sagitta, tovuti ya Ian Ridpath, iliangaliwa Oktoba 2017
- The Deep Photographic Guide to the Constellations: Sagitta
MarejeoEdit
- Richard Hinckley Allen: Star-Names and their Meanings; kwa G. E. Stechert New York, Leipzig, London, Paris 1899, “Argo Navis” ukurasa 131 ff (online hapa kwenye archive.org)
- Jan Knappert, 1993: The Swahili Names of Stars, Planets and Constellations; The Indian Ocean Review September 1993 Volume 6 No. 3 September 1993, kurasa 6-7, ISSN 1031-2331
Dunia: iko katikati
zinafuata mizingo ya Lunae (Mwezi), Mercurii (Utaridi), Veneris (Zuhura), Solis (Jua),
halafu ya Martis (Mirihi), Iovis (Mshtarii) na Saturni (Zohali)
halafu Octavum Firmamentum (mbingu wa nane), halafu Nonum Coelum Cristalinum (mbingu wa tisa, wa kioo),
Coelum Empireum Habitaculum Dei et Omnium Electorum (Mbingu wa moto, mahali pa Mungu na wa wote waliochaguliwa naye