Selulitisi (kutoka Kilatini na Kiingereza: "cellulitis") ni ugonjwa unaotokana na bakteria unaoathiri undani wa ngozi.

Dalili zake ni pamoja na ngozi kubadilika rangi kuwa nyekundu na pia kuvimba. Sehemu iliyoathiriwa huwa na maumivu. [1]

Mgonjwa anaweza kuwa na homa na kujisikia mchovu.[2]

Miguu na uso ndio sehemu zinazoathiriwa zaidi na ugonjwa huu ingawa unaweza kuathiri sehemu yoyote ya mwili.

Kati ya sababu zinazofanya mtu kupata ugonjwa huu ni pamoja na unene kupita kiasi, kuvimba kwa miguu, na uzee. Bakteria wanaosababisha ugonjwa huu ni streptococci na Staphylococcus aureus.

Matibabu yake huwa ni kwa dawa kama vile cephalexin, amoxicillin au cloxacillin. Kwa wale wenye matatizo ya kutumia dawa kama penicillin, dawa za erythromycin na clindamycin hutumiwa.

Wengi sana wanapona bada ya siku 7-10 za kutumia dawa kama hizo.

Picha hariri

Marejeo hariri

  1. Tintinalli, Judith E. (2010). Emergency Medicine: A Comprehensive Study Guide (Emergency Medicine (Tintinalli)) (toleo la 7th). New York: McGraw-Hill Companies. uk. 1016. ISBN 978-0-07-148480-0. 
  2. Mistry, RD (Oct 2013). "Skin and soft tissue infections". Pediatric Clinics of North America 60 (5): 1063–82. PMID 24093896. doi:10.1016/j.pcl.2013.06.011. 

Soma zaidi hariri

  • Stevens, DL; Bisno, AL; Chambers, HF; Dellinger, EP; Goldstein, EJ; Gorbach, SL; Hirschmann, JV; Kaplan, SL; Montoya, JG; Wade, JC (15 July 2014). "Practice guidelines for the diagnosis and management of skin and soft tissue infections: 2014 update by the infectious diseases society of America.". Clinical Infectious Diseases 59 (2): 147–59. PMID 24947530. doi:10.1093/cid/ciu296.  Check date values in: |date= (help)
  Makala hii kuhusu mambo ya tiba bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Selulitisi kama sababu yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.