Sifa za Bikira Maria

Sifa za Bikira Maria zinapatikana katika madhehebu mbalimbali ya Kikristo na katika Uislamu, akiwa mwanamke pekee anayetajwa kwa jina na Kurani. Zote zinategemea ukweli wa msingi kwamba ndiye mzazi wa Yesu.

Bikira Maria na Mtoto Yesu kati ya watakatifu za Ethiopia; picha takatifu za katikati ya karne ya 17.

Zile muhimu zaidi zinafuata moja kwa moja imani ya madhehebu hayo, baadhi ni namba za kumuitia katika sala, baadhi tena ni za kisanii katika kumfananisha na viumbe vingine. Pia kuna sifa zinazotokana na uchoraji na sanaa kwa jumla kumhusu yeye.