Sucre ni mji mkuu wa kikatiba wa Bolivia na makao ya Mahakama Kuu ya nchi. Iko kwenye kusini ya nchi kwa kimo cha takriban mita 3,000 katika mkoa wa Chuquisaca. Idadi ya wakazi ni karibu watu 250,000 (2006).

Sucre,Bolovia
Sucre

Mji wa Kale wa Sucre
Habari za kimsingi
Utawala Mkoa wa Chuquisaca
Historia imeundwa 29 Septemba 1538 kwa jina "Ciudad de la Plata de la Nueva Toledo" (mji wa fedha wa Toledo mpya)
Anwani ya kijiografia Latitudo: 19°2′34"S
Longitudo: 65°15′19"W
Kimo 2,904 m juu ya UB
Eneo ? km²
Wakazi - mji: 247,300 (2006)
Msongamano wa watu watu ? kwa km²
Simu +591 (nchi yote) 4 (mji)
Mahali

Mji uliundwa 1539 kwa jina la Ciudad de la Plata de la Nueva Toledo (mji wa fedha wa Toledo mpya" kwa kumbukumbu ya utajiri wa migodi ya fedha pia kwa heshima ya mji wa Toledo (Hispania). Ilitwa pia kifupi "La Plata" au "Charcas". 1839 ilikuwa mji mkuu wa nchi mpya ya Bolivia ikapewa jina mpya la Sucre kwa heshima ya kiongozi wa mapambano ya uhuru dhidi ya Hispania Antonio José de Sucre.

Baada ya kuchoka kwa migodi ya fedha katika sehemu hii ya nchi serikali na bunge ziliondoka Sucre kwenda La Paz kwa sababu ya mawasiliano magumu na sehemu nyingine ya nchi. Mahakama Kuu ilibaki.

Majengo mengi ya kihistoria yamehifadhiwa. Sucre inatazamaiwa kama mfano bora wa mji wa Kihispania katika Amerika ya Kilatini. UNESCO imeandikisha mji katika orodha lake la "urithi wa dunia".

Makala hii kuhusu maeneo ya Bolivia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Sucre kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.