Carl Velten

(Elekezwa kutoka Velten)

Carl Velten (1862–1935) alikuwa mtaalamu wa lugha katika Ujerumani aliyekusanya hadithi na desturi nyingi za Waswahili na kutunga Kamusi ya Kiswahili-Kijerumani kabla ya vita kuu ya kwanza ya dunia wakati wa Afrika ya Mashariki ya Kijerumani.

Velten mzee

Velten alizaliwa 4 Septemba 1862 katika kijiji cha Fluterschen, wilaya ya Altenkirchen kwenye mkoa wa Rhine ya Prussia. 1888-1885 alisoma lugha kwenye vyuo vikuu va Bonn na Tübingen. Baada ya masomo alisafiri kutembelea Ufaransa, Uingereza, Algeria, Tunisia na Misri. Alijiandaa kwa utumishi wa serikali ya Ujerumani katika koloni kwa masomo kwenye chuo cha lugha za mashariki Berlin.

Kazi yake katika Afrika ya Mashariki hariri

1893 hadi 1896 alikuwa mkalimani au mfasiri wa serikali ya kijerumani ya Afrika ya Mashariki. Katika miaka ile alikusanya fasihi simulizi ya wenyeji kama vile masimulizi, hadithi, mila na desturi nyingi. Aliandika maneno ya wasimulizi wake kwa shorthand. Aliajiri pia wasomi kutoka miji ya Waswahili akawaomba kuandika mapokeo ya kihistoria, kwa mfano historia za Lindi, Mikindani na Sudi[1]. 1896 akarudi Ujerumani kuwa profesa wa Kiswahili kwenye chuo cha lugha za mashariki cha chuo kikuu cha Berlin. Alimkaribisha Mtoro bin Mwinyi Bakari kuja naye Berlin na huyu aliendelea kuwa mshauri wake Velten alipohariri maandiko yake juu ya Waswahili.

Maandiko yake hariri

Sehemu ya vitabu vyake alitoa kwa Kiswahili na Kijerumani vilevile. Hivi ni hasa kuhusu masimulizi, mila na desturi alizokusanya wakati wa kufanya kazi Afrika ya Mashariki.

  • Hadithi na Mazimulizi ya Waswahili - Märchen und Erzählungen der Suaheli (Suahelitext: Band XVIII der Lehrbücher des Oriental. Seminars), Berl. 1898
  • (Sarufi ya Kinyamwezi) Grammatik des Kinyamuesi, der Sprache der Wanyamuesi in Deutsch-Ostafrika nebst Wörterverzeichnis, 1901
  • (Mwongozo kwa kujifunza maandishi ya Kiarabu ya Waswahili) Praktische Anleitung zur Erlernung der arabischen Schrift der Suaheli, Gött. 1901
  • Safari za Wasuaheli, Gött. 1901 / Reiseschilderungen der Suaheli, Gött. 1901
  • Desturi za Wasuaheli na khabari za desturi za sheri'a za Wasuaheli, Gött. 1903; Sitten und Gebräuche der Suaheli nebst Rechtsanschauungen, Gött. 1903
  • (Hadithi na Shairi za Waswahili) Prosa und Poesie der Suaheli, Berl. 1907; (pamoja na historia za Lindi, Mikindani na Sudi; online hapa
  • (Sarufi ya Kiswahili) Praktische Suaheli-Grammatik nebst einem Deutsch-Suaheli - Wörterverzeichnis, 3. Aufl., Berl. 1910
  • (Kamusi ya Kiswahili-Kijerumani) Suaheli-Wörterbuch, 1. Teil, Suaheli-Deutsch, Berl. 1910
  • (Mwongozo wa Kiswahili kwa ajili ya watumishi wa posta) Suaheli-Sprachführer für Postbeamte, Berl. 1910
  • (Kamusi ndogo ya Kiswahili-Kijerumani na Kijerumani-Kiswahili) Taschenwörterbuch der Suaheli-Sprache, Suaheli-Deutsch und Deutsch-Suaheli, Berl. 1911
  • (Desturi za Waswahili) Gebräuche der Suaheli, 1898
  • (Maelezo juu ya majina ya mahali katika Afrika ya Mashariki) Erklärung einiger ostafrikanischer Ortsnamen, 1898
  • (Lugha ya Wahehe) Die Sprache der Wahehe, Grammatik und Wörterbuch, 1899
  • (Lugha ya Kikami) Kikami, die Sprache der Wakami in Deutsch-Ostafrika, 1900
  • (Majina ambayo Wazungu wanapewa na Waswahili) Die Spitznamen der Europäer bei den Suaheli, 1900;
  • (Vitendawili 100 vya Waswahili) Hundert Suaheli - Rätsel, 1904.

Marejeo hariri

  1. Pawlowicz M. and LaViolette, A. 2013. Swahili Historical Chronicles from an Archaeological Perspective: Bridging History and Archaeology, and Coast and Hinterland, in Southern Tanzania. In P. Schmidt and S. Mrozowski (Eds.), The Death of Prehistory (pp. 117-140). Oxford: Oxford University Press. online hapa