Tunisia
Tunisia, rasmi kama Jamhuri ya Tunisia (kwa Kiarabu الجمهرية التونسية, al-Jumhūrīya at-Tūnisīya), ni nchi katika Afrika Kaskazini, inayopakana na Bahari ya Mediteranea kaskazini na mashariki, Aljeria magharibi, na Libya kusini-mashariki. Ina idadi ya watu takriban milioni 12, ikiwa ya 79 duniani. Jiji lake kubwa zaidi ni Tunis, ambalo pia ni mji mkuu. Tunisia imegawanyika katika majimbo 24 yanayosimamia utawala wa ndani. Inajulikana kwa makazi ya ustaarabu wa Karthago.
Jamhuri ya Tunisia الجمهورية التونسية | |
---|---|
Wimbo wa taifa: "Humat Al-Hima" | |
Mji mkuu na mkubwa | Tunis |
Lugha rasmi | Kiarabu |
Kabila (2021) | 98% Waarabu 1% Waberber 1% Wayahudi na wengine |
Serikali | Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kiraia |
• Rais | Kais Saied |
• Waziri Mkuu | Kamel Madouri |
Historia | |
• Kuanzishwa kwa Karthage | 814 KK |
• Utawala wa Husainid | 15 Julai 1705 |
• Uhuru kutoka Ufaransa | 20 Machi 1956 |
• Kutangazwa kwa Jamhuri | 25 Julai 1957 |
Eneo | |
• Jumla | km2 163,610 km² (ya 91) |
• Maji (asilimia) | 5.04% |
Idadi ya watu | |
• Kadirio la 2020 | ▲ 11,708,370 |
• Msongamano | 71.65/km2 |
PLT (PPP) | Kadirio la 2023 |
• Jumla | ▲ $162.097 bilioni (ya 82) |
• Kwa kila mtu | ▲ $13,248(ya ) |
PLT (Kawaida) | Kadirio la 2023 |
• Jumla | ▲ $51.271 bilioni |
• Kwa kila mtu | ▲ $4,190 |
HDI (2022) | 0.732 |
Sarafu | Dinar ya Tunisia (TND) |
Majira ya saa | UTC+1 CET |
Upande wa magari | Kulia |
Msimbo wa simu | +216 |
Jina la kikoa | .tn |
Historia
haririTunisia iliwahi kutawaliwa na Wafinikia walioanzisha huko mji wa Karthago.
Baada ya hao kushindwa na Roma ya Kale, ilikuwa jimbo la Afrika katika Dola la Roma.
Kisha eneo lake likatawaliwa kwa awamu na Wavandali, Waarabu, Wahispania, Waturuki na Wafaransa.
Watu
haririWakazi karibu wote (98%) wanajiita Waarabu na hutumia lugha ya Kiarabu ambacho ndicho lugha rasmi. Hata hivyo damu yao ni mchanganyiko hasa wa ile ya Waberber, Waarabu na Waturuki.
Takriban watu 200,000, hasa kusini, wanaendelea kuzungumza Kiberber ambacho ni lugha asili ya wenyeji lakini Waberber wengi wamezoea kutumia Kiarabu.
Katika elimu na biashara Kifaransa kinatumika pia sana.
Upande wa dini, Uislamu unafuatwa na asilimia 99 za wakazi, nao ndio dini rasmi, lakini theluthi moja kati yao, na nusu kati ya vijana, wanajitambulisha kama wasio na dini, kiwango kikubwa kuliko nchi zote za Kiarabu. Waliobaki ni Wakristo, hasa Wakatoliki, na Wayahudi wachache.
Tazama pia
haririViungo vya nje
hariri- Government of Tunisia (official website).
- Tunisia entry at The World Factbook
- Tunisia katika Open Directory Project
- Tunisia profile from BBC News.
- Wikimedia Atlas of Tunisia
Nchi za Afrika | |
---|---|
Afrika ya Kati (Jamhuri ya) | Afrika Kusini | Algeria | Angola | Benin | Botswana | Burkina Faso | Burundi | Cabo Verde | Chad | Cote d'Ivoire | Eritrea | Eswatini | Ethiopia | Gabon | Gambia | Ghana | Guinea | Guinea Bisau | Guinea ya Ikweta | Jibuti | Kamerun | Kenya | Komori | Kongo (Jamhuri ya) | Kongo (Jamhuri ya Kidemokrasia ya) | Lesotho | Liberia | Libya | Madagaska | Malawi | Mali | Misri | Morisi (Visiwa vya) | Mauritania | Moroko | Msumbiji | Namibia | Niger | Nigeria | Rwanda | Sahara ya Magharibi | Sao Tome na Principe | Senegal | Shelisheli | Sierra Leone | Somalia | Sudan | Sudan Kusini | Tanzania | Togo | Tunisia | Uganda | Zambia | Zimbabwe | |
Maeneo ya Afrika ambayo ni sehemu za nchi nje ya Afrika | |
Hispania: Kanari · Ceuta · Melilla | Italia: Pantelleria · Pelagie | Ufaransa: Mayotte · Réunion | Uingereza: · St. Helena · Diego Garcia | Ureno: Madeira |
Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Tunisia kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |