Rhine (tamka: rain) (kwa Kijerumani Rhein, Kifaransa Rhin na Kiholanzi Rijn) ni kati ya mito mirefu ya Ulaya.

Rhine (Rhein)
Rhine katika Ujerumani kwenye mwamba wa Loreley
Chanzo Grisons (Uswisi)
Mdomo Bahari ya Kaskazini katika Uholanzi
Nchi Uswisi, Liechtenstein, Austria, Ujerumani, Ufaransa, Uholanzi
Urefu 1,230 km
Kimo cha chanzo 2,344 m
Tawimito upande wa kulia Neckar, Main, Lahn, Ruhr, Lippe
Tawimito upande wa kushoto Aare, Ill, Mosel
Mkondo 2230 m³/s
Eneo la beseni 185,000 km²
Miji mikubwa kando lake Basel, Strassburg, Karlsruhe, Mannheim, Ludwigshafen, Wiesbaden, Mainz, Koblenz, Bonn, Köln, Leverkusen, Düsseldorf, Neuss, Krefeld, Duisburg, Nimwegen, Rotterdam, Arnheim, Utrecht, Leiden

Chanzo na nchi inapopita hariri

 
Ramani ya Rhine

Ina chanzo chake katika milima ya Uswisi. Inapita katika Uswisi, Ujerumani na Uholanzi; mwendo wake ni pia mpaka kati ya Uswisi na Liechtenstein, Uswisi na Austria halafu Ujerumani na Ufaransa.

Mpakani kati ya Uswisi na Ujerumani mto inapita katika ziwa la Konstanz (au: Bodensee).

Njia ya maji hariri

Kuanzia mji wa Rheinfelden hadi Rotterdam kwa urefu wa zaidi ya 800 km mto unapitika kwa meli za mtoni.

Usafiri mtoni ni muhimu kwa ajili ya viwanda vingi vilivyopo kando la mto.

Kihistoria Rhine pamoja na mto Danubi ilikuwa mpaka wa kakazini ya Dola la Roma.

Delta ya Rhine hariri

Ndani ya Uholanzi mto hujigawa kuwa na mikono mikubwa miwili inayoitwa Waal na Lek. Mbele ya mji wa Rotterdam inaungana tena kuwa mto mmoja.

 
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:


  Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Rhine kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.