Kucha wa Afrika

(Elekezwa kutoka Achaetops)
Kucha wa Afrika
Kikucha uso-mwekundu
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Passeriformes (Ndege kama shomoro)
Familia ya juu: Sylvioidea (Ndege kama kucha)
Familia: Macrosphenidae (Ndege walio na mnasaba na kolojojo)
Wolters, 1983
Ngazi za chini

Jenasi 6, spishi 18:

Kucha wa Afrika ni ndege wadogo ambao zamani waliainishwa katika Sylviidae, familia ya kucha wengine. Sasa wataalamu wanakubaliana kwamba ndege hawa ni kundi lao lenyewe pamoja na vikucha na kolojojo. Kwa hivyo wamepata familia yao Macrosphenidae. Kucha wa Afrika bila vikucha na kolojojo wanafanana na shoro, kuchanyika na kuchamsitu ambao zamani waliainishwa pia katika familia Sylviidae. Wana mkia mrefu kiasi na rangi yao ni kahawia au kahawianyekundu. Wana michirizi mizito kujumuisha “masharubu”, isipokuwa kucha wa Victorin. Vikucha na kolojojo wana mkia mfupi.

Hula wadudu ambao huwatafuta ardhini, chini ya uoto au katika gome la miti. Hulijenga tago lao kwa umbo wa kikombe katika miti au ndani ya uoto mzito, mara nyingi karibu na ardhi. Jike huyataga mayai 2-5.

Spishi za Afrika hariri

Picha hariri