Abedi Amani Karume

(Elekezwa kutoka Amaan Karume)

Sheikh Abeid Amani Karume alikuwa Rais wa kwanza wa Zanzibar. Alizaliwa mwaka 1905 na kufariki tarehe 7 Aprili 1972 kwa kupigwa risasi.

Karume

Karume aliongoza nchi baada ya mapinduzi yaliyomwangusha Sultani aliyekuwa akitawala Zanzibar hadi mwanzoni mwa mwaka 1964.

Baada ya miezi mitatu Zanzibar iliungana na Tanganyika iliyokuwa ikiongozwa na Mwalimu Nyerere. Baada ya muungano wa nchi hizi mbili uliozaa Tanzania, Karume alikuwa makamu wa rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Amani Abeid Karume, ambaye ni mtoto wa Sheikh Karume, alikuwa rais wa Zanzibar tangu mwaka 2000 hadi 2010.

Alitanguliwa na
Nafasi ilivyoundwa
Makamu wa Rais wa Tanzania
1964-1972
Akafuatiwa na
Mwinyi Aboud Jumbe