Barsimeo wa Edessa

Barsimeo wa Edessa (pia: Barsamya) alikuwa askofu wa Edessa, leo Urfa, nchini Uturuki.

Aliwahi kupigwa fimbo kutokana na dhuluma ya kaisari Decius (249-251) lakini hakuuawa, bali alirudi jimboni mwake na kuliongoza kwa bidii hadi kifo chake[1]. Kati ya watu aliowaongoa kuna Sharbel na Bebaya.

Tangu kale anaheshimiwa na Waorthodoksi na Wakatoliki kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 30 Januari[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.