Boda boda (pia: bodaboda au "baisikeli ya teksi") ni baisikeli au pikipiki inayotumiwa kubeba abiria katika Afrika ya Mashariki. Linaweza kumtaja pia dereva wake.

Boda boda njiani
Kiti cha boda boda

Historia hariri

Asili yake ni kati ya Wajaluo wa eneo la mpakani kati ya Kenya na Uganda karibu na ziwa Viktoria. Inasemekana asili yake ilikuwa huduma ya kubeba abiria kati ya mipaka ya Kenya na Uganda mjini Busia. Hivyo neno la Kiingereza la "border" = "boda" lilikuwa chanzo cha jina "boda-boda". Halafu huduma imeenea sehemu mbalimbali.

Baisikeli ya kawaida inayotakiwa imara hubadilishwa kwa kuweka kiti kirefu kama cha pikipiki.

Baadaye kulitokea badiliko ambapo pikipiki zinachukua nafasi za baiskeli katika kazi ya kubeba abiria. Kuna makadirio kuhusu mwaka 2004 ya kuwa watu 200,000 Uganda walikuwa madereva wa boda boda ya baisikeli na 90,000 wa boda boda ya pikipiki.

Ajali na matatizo hariri

Baada ya wengi kuacha baiskeli na kukimbilia pikipiki kwa ajili ya boda boda, kumekuwa na ongezeko kubwa la ajali barabarani. Karibu kila siku watu wanafariki kwa ajali za namna hiyo. Bodaboda wamekuwa pia chanzo cha uharibifu wa ndoa za watu, ubebaji wa bidhaa haramu, uchafuzi wa mazingira, na vijana wengi kuwa na imani potofu kuwa bodaboda ndiyo shule, hivyo hawana haha ya kusoma. Hii imepelekea watu wengi kuona bodaboda ni kazi inayofanywa na vijana wahuni waliokosa maadili.

Viungo vya nje hariri