Dogma ni neno linalotumika hasa kumaanisha fundisho la imani lisiloweza kukanushwa na wafuasi wa dini fulani. Linaweza kutumika pia kwa maana isiyo ya kidini.

Asili ya neno hariri

Neno la Kigiriki δογμα, dògma, linatokana na kitenzi δοκω, doko. Maana zake zilikuwa tatu:

1. rai;

2. wazo, fundisho la falsafa au dini;

3. uamuzi, tamko.

Katika Kanisa Katoliki hariri

"Dogma ya imani" inamaanisha tamko lililotolewa na Mtaguso Mkuu au Papa kwa niaba ya maaskofu wote kumalizia mjadala kuhusu fundisho fulani baada ya kuthibitisha ufunuo wa Mungu unasema nini juu ya hilo.

Baada ya hapo, mwamini anayekataa dogma anahesabiwa kuwa mzushi na kutengwa na Kanisa Katoliki.