Franco Anelli (26 Juni 196323 Mei 2024) alikuwa msomi na mkuu wa chuo kikuu kutoka Italia.

Anelli 2021

Wasifu

hariri

Anelli alizaliwa mjini Piacenza tarehe 26 Juni 1963. Alikuwa profesa wa sheria ya kibinafsi kuanzia mwaka 1993. Alihitimu shahada ya sheria katika Chuo Kikuu Katoliki cha Sacred Heart (Università Cattolica del Sacro Cuore). Baada ya kupata shahada ya uzamivu (PhD) katika sheria ya kibiashara, alikua profesa mshiriki wa taasisi za sheria ya kibinafsi katika Kitivo cha Uchumi na Biashara. Alijihusisha zaidi na sheria za wajibu na mikataba pamoja na haki za mali katika familia. Pia alisasisha Kitabu cha Mwongozo wa Sheria ya Kibinafsi cha Torrente-Schlesinger kilichochapishwa na Giuffrè. Aliteuliwa kuwa mkuu wa chuo cha Università Cattolica mnamo Desemba 2012.[1] Anelli alijiua kwa kujitupa huko Milan, tarehe 23 Mei 2024, akiwa na umri wa miaka 60.[2]

Marejeo

hariri
  1. "Cattolica, Franco Anelli nuovo rettore"Avanti fra tradizione e innovazione"". 12 Desemba 2012.{{cite web}}: CS1 maint: date auto-translated (link)
  2. "Franco Anelli, morto il rettore dell'Università Cattolica. Si è ucciso gettandosi dal sesto piano a Milano", Il Messaggero, 24 May 2024. 
  Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Franco Anelli kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.