Shore (Muscicapidae)

(Elekezwa kutoka Fraseria)
Shore
Shore kijivucheusi
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Passeriformes (Ndege kama shomoro)
Familia ya juu: Muscicapoidea (Ndege kama shore)
Familia: Muscicapidae (Ndege walio na mnasaba na shore)
Nusufamilia: Muscicapinae (Ndege wanaofanana na shore)
Ngazi za chini

Jenasi 14:

Shore, shorwe au sholwe ni ndege wadogo wa nusufamilia Muscicapinae katika familia Muscicapidae. Spishi nyingine zinaitwa chekiro, kidaku au gongo shaba. Spishi kadhaa za familia Pycnonotidae zinaitwa shore pia. Wale wa Muscicapinae wana rangi ya kahawa, kijivu au nyeusi kwa kawaida, lakini spishi nyingine wana rangi kali kama buluu, nyekundu, manjano na machungwa. Shore wanatokea misitu na maeneo mengine yenye miti katika Afrika na Asia. Hula wadudu. Kwa kawaida shore hukaa tawi wakiangalia ujirani. Wakiona mdudu huruka ili kumkamata na kurudi tawi. Hujenga tago lao kwa umbo wa kikombe katika tundu la mti au dhidhi ya shina. Jike huyataga mayai 2-6.

Spishi za Afrika hariri

Spishi wa Asia hariri

Picha hariri