Fuko (Bathyergidae)

(Elekezwa kutoka Georychus)
Fuko
Fuko wa Damaraland (Fukomys damarensis)
Fuko wa Damaraland (Fukomys damarensis)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mammalia (Wanyama wenye viwele)
Oda: Rodentia (Wanyama wagugunaji)
Familia: Bathyergidae (Wanyama walio na mnasaba na fuko-mchanga)
Waterhouse, 1841
Ngazi za chini

Jenasi 6:
Bathyergus Illiger, 1811
Cryptomys Gray, 1864
Fukomys Kock et al., 1906
Georychus Illiger, 1811
Heliophobius Peters, 1846
Heterocephalus Rüppell, 1842

Mafuko hawa ni wanyama wa familia Bathyergidae ambao wanachimba katika ardhi na kushinda takriban maisha yao yote chini ya uso wake. Wanyama wengine waitwao fuko ni wanafamilia wa Chrysochloridae (oda Afrosoricida), Spalacidae (Rodentia), Talpidae (Soricomorpha) na Notoryctidae (Notoryctemorphia). Spishi zote za Bathyergidae zinatokea Afrika kusini kwa Sahara. Hula mizizi, matunguu na viazi. Kwa hivyo wanyama hawa wana meno manne makubwa mbele mdomoni. Huyatumia meno haya pia kwa kuchimba mahandaki yao. Macho na masikio yao ni madogo na mkia vilevile. Wamepoteza nusra uwezo wa kuona, lakini angalau spishi mbili wanaweza kuhisi nuru. Manyoya yao ni kama bahameli na yana rangi ya kahawia au hudhurungi, lakini fuko uchi hana manyoya. Takriban spishi zote huishi peke yao lakini fuko uchi na fuko wa Damaraland ni mamalia wa pekee ambao huishi kwa jamii za aina ya eusocial kama nyuki au mchwa. Jike mmoja na dume mmoja tu huzaa; wanyama wengine wa jamii ni gumba na husaidia kwa kutafuta chakula na kutunza makinda.

Spishi hariri

Picha hariri

Marejeo hariri

  1. Gippoliti, S. & Amori, G. (2011). "A new species of mole-rat (Rodentia, Bathyergidae) from the Horn of Africa". Zootaxa 2918: 39–46.