Regina McCarthy (alizaliwa Mei 3, 1954) ni mtaalamu wa hali ya hewa kutoka Marekani ambaye aliwahi kuwa mshauri wa kwanza wa hali ya hewa wa Ikulu ya White House kutoka mwaka 2021 hadi 2022. Hapo awali alikuwa Msimamizi wa kumi na tatu wa Shirika la Ulinzi wa Mazingira kutoka mwaka 2013 hadi 2017[1].

Regina McCarthy nimzaliwa wa Massachusetts, McCarthy ana shahada kutoka Chuo Kikuu cha Massachusetts Boston na Chuo Kikuu cha Tufts. Alikuwa mtumishi wa umma katika serikali ya jimbo la Massachusetts, akishikilia majukumu mbalimbali ya mazingira na kutumika kama mshauri wa mazingira kwa Gavana wa Massachusetts. Alihudumu kama kamishna wa Idara ya Ulinzi wa Mazingira ya Connecticut kutoka mwaka 2004 hadi 2009 kabla ya kujiunga na EPA mnamo 2009.[2]

Marejeo hariri

  1. Friedman, Lisa (2022-09-02), "Gina McCarthy, Biden’s Top Climate Adviser, to Step Down Sept. 16", The New York Times (kwa en-US), ISSN 0362-4331, iliwekwa mnamo 2023-04-09 
  2. "Gina McCarthy". The Institute of Politics at Harvard University (kwa Kiingereza). Iliwekwa mnamo 2023-04-09. 
  Makala hii kuhusu mwanasayansi fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Gina McCarthy kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.