Jang Bogo

Mtawala wa Korea

Jang Bogo (787846), jina lake la utotoni aliitwa Gungbok, alikuwa mtu kutoka ufalme wa Silla (kusini na katikati ya peninsula ya Korea) ambaye alikuja kuwa maarufu na muhimu sana katika Silla ya baadaye, wakati ambapo Korea ilikuwa nchi yenye nguvu sana, hasa upande wa shughuli za kijeshi za majini (jeshi la majini) ambaye aliiratibu vizuri mno bahari inayoitwa Yellow Sea, mashariki mwa nchi hiyo,[1] na alitawala shughuli za biashara kati ya Silla, Heian Japan, na Tang China kwa miongo kadhaa.[2].

Makundi ya meli zake za kustaajabisha zilikuwa katika kisiwa cha Wando kisiwa kilichokuwa kusini mwa jimbo la Jeolla (South Jeolla Province).Kadiri alivyozidi kuvuta hisia za watu na kukonga nyoyo zao, Jang Bogo alipewa ofisi na kuwa Kamishina wa shughuli zilizohusha bahari (Kamishina wa majini) katika makao makuu ya kijeshi iliyokuwa katika kisiwa cha Wando kusini mwa jimbo la Jeolla.Baadaye alimuozesha binti yake katika familia ya kifalme kabla hajauliwa mnamo mwaka 846 B.K.

Marejeo hariri

  1. Tagliacozzo, Eric. Asia Inside Out (kwa Kiingereza). Harvard University Press. ISBN 9780674286344. Iliwekwa mnamo 17 March 2017.  Check date values in: |accessdate= (help)
  2. Shin, Gi-Wook; Choi, Joon. Global Talent: Skilled Labor as Social Capital in Korea (kwa Kiingereza). Stanford University Press. uk. 68. ISBN 9780804794381. Iliwekwa mnamo 17 March 2017.  Check date values in: |accessdate= (help)