Kidugala ni jina la kata ya Wilaya ya Wanging'ombe katika Mkoa wa Njombe, Tanzania. Wakati wa wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 4,838 [1] walioishi humo. Msimbo wa posta ni 59312.

Wakazi wa Kidugala ni Wabena.

Mwanzo wa misioni ya Kiluteri Edit

Katika karne ya 19 kulikuwa hapa na makao makuu ya Mwene Ngele (au Ngera). Huyu alikaribisha Wamisionari wa Shirika la Misioni ya Kiluteri ya Berlin walioanzisha hapa kituo chao kwenye mwaka 1898. Kutoka hapa Kidugala iliendelea kuwa kitovu cha misioni ya Kiluteri katika Ubena. Mwaka 1904 Wamisionari walianzisha shule kwa ajili ya wainjilisti iliyoendelea kuwa chuo cha Biblia baadaye. Kanisa lilijengwa 1908, karahana ya kuchapa vitabu 1910. Mwaka 1911 hospitali ya misioni ilikamilika. 1914 ushirika wa kiluteri ulikuwa na Wakristo 114 na Wakatekumeni 71.[2]

Tanbihi Edit

  1. Sensa ya 2012, Njombe - Wanging'ombe DC. Jalada kutoka ya awali juu ya 2004-01-02. Iliwekwa mnamo 2017-03-28.
  2. Altena, uk. 180

Marejeo Edit

  • Thorsten Altena: "Ein Häuflein Christen mitten in der Heidenwelt des dunklen Erdteils". Zum Selbst- und Fremdverständnis protestantischer Missionare im kolonialen Afrika 1884-1918 (= Internationale Hochschulschriften; Bd. 395), Münster: Waxmann 2003, 531 S., 12 Abb., 1 CD-Rom, ISBN 3-8309-1199-8
  Kata za Wilaya ya Wanging'ombe - Tanzania  

Igima | Igosi | Igwachanya | Ilembula | Imalinyi | Kidugala | Kijombe | Kipengele | Luduga | Makoga | Mdandu | Saja | Uhambule | Ulembwe | Usuka | Wangama | Wanging'ombe


  Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Njombe bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Kidugala kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.