Kiwikalkan (pia Kiwik-Ngatharr au Kiwik-Alken) ni lugha ya Kipama-Nyungan nchini Australia inayozungumzwa na Wawik katika jimbo la Queensland. Mwaka wa 1981, idadi ya wasemaji wa Kiwikalkan ilihesabiwa kuwa watu 86 tu, na wasemaji wengi wameacha lugha yao ya kwanza na kutumia Kiwik-Mungkan. Kwa hiyo, Kiwikalkan imo hatarini mwa kutoweka kabisa. Kufuatana na uainishaji wa lugha kwa ndani zaidi, Kiwikalkan kiko katika kundi la Kipama cha Kati. Wengine huiangalia kama lahaja ya Kiwik-Ngathana.

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kiwikalkan kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.