Kubwilu
Kubwilu manjano
Kubwilu manjano
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Passeriformes (Ndege kama shomoro)
Familia ya juu: Corvoidea (Ndege kama kunguru)
Familia: Oriolidae (Ndege walio na mnasaba na kubwilu)
Jenasi: Oriolus Linnaeus, 1766

Sphecotheres Vieillot, 1816

Spishi: Angalia katiba.

Kubwilu, kubwiro au naiwa ni ndege wa familia Oriolidae. Wanatokea Afrika, Asia, Australia na Ulaya. Spishi nyingi zina rangi za manjano na nyeusi, lakini nyingine zina rangi za majani, nyekundu au kahawa pamoja na nyeusi. Ndege hawa wana sauti tamu bainifu. Hula matunda, beri na arithropodi. Hulijenga tago lao kwa umbo wa kikombe kilichofuma na hili limening'inizwa kutoka tawi kama susu. Jike huyataga mayai 2-3, hata hadi 6.

Spishi za Afrika hariri

Spishi za mabara mengine hariri

Picha hariri