La Verna, kwa Kilatini Alverna na kijiografia Monte Penna, ni mlima unaosimama peke yake hadi mita 1,283 katikati ya Apenini ya Toscana, juu ya bonde la Casentino, Italia ya Kati.

Basilika la patakatifu pa La Verna.

Ni maarufu hasa kwa sababu inasemekana Fransisko wa Asizi, akiwa kwenye mfungo mkali juu yake miezi ya Agosti na Septemba 1224, alipata njozi ya Yesu msulubiwa aliyemtia mwilini madonda yake matano.

Baadaye palijengwa patakatifu panapovutia watu wengi. Mnamo Agosti 1921 Papa Benedikto XV alipatangaza basilika dogo.[1]

Tanbihi hariri

  1. Catholic.org - Basilicas in Italy

Viungo vya nje hariri

 
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu La Verna kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Coordinates: 43°42′25″N 11°55′52″E / 43.707°N 11.931°E / 43.707; 11.931