Maungano ya kifalme

Maungano ya kifalme ni hali ya kisiasa na kisheria ambako nchi mbili zinashirikiana mtu yuleyule kama mfalme wao au mkuu wa dola.

Nchi zote mbili zinaendelea kuwa madola ya pekee lakini mfalme ni yeye yule.

Maungano ya aina hii hupatikana katika utaratibu wa utawala wa kifalme lakini haipatikani katika utaratibu wa kijamhuri.

Wakati wa kisasa hariri

Jumuiya ya Madola hariri

Mifano ni siku hizi hasa Jumuiya ya Madola. Nchi nyingi za jumuiya hii zinamtambua malkia Elizabeth II kama mkuu wa dola kufuatana na katiba ya nchi. Malkia anamteua gavana mkuu kama mwakilishi wake nchini. Katika utaratibu huu nchi hizi zitamtambua pia mfalme au malkia atakayemfuata Elizabeth II kufuatana na sheria za Uingereza kuwa mkuu mpya wa nchi yao.

Andorra hariri

Nchi ndogo ya Andorra kati ya Ufaransa na Hispania ni mfano wa pekee ambako rais wa jamhuri anakuwa mkuu wa dola wa nchi nyingine. Tangu mwaka 1607 nafasi ya mkuu wa dola wa Andorra hushirikishwa kati ya askofu wa Urgel (Hispania) na mfalme wa Ufaransa. Baada ya mapinduzi ya Ufaransa mwaka 1789 rais wa jamhuri alichukua nafasi ya mfalme wa awali.

Mifano ya kihistoria hariri

Historia ina mifano mingi ya maungano ya kifalme kati ya nchi mbili zilizoendelea na taratibu zao za pekee lakini kumshirikiana mfalme yeye yule.

  Makala hiyo kuhusu "Maungano ya kifalme" inatumia neno ambalo si kawaida na matumizi yake ni jaribio kwa jambo linalotajwa.
Wasomaji wanaombwa kuchangia mawazo yao.

Kamusi za Kiswahili ama zinatofautiana kuhusu matumizi ya neno hili au hazieleweki au hazina neno kwa jambo linalojadiliwa.