Israel
Israel (kwa Kiebrania: מדינת ישראל - Medinat Yisra'el; kwa Kiarabu: دَوْلَةْ إِسْرَائِيل - dawlat Isrā'īl) , rasmi Dola la Israel, ni nchi iliyoko Magharibi mwa Asia. Iko katika eneo la Kusini mwa Levant katika Mashariki ya Kati; na inapakana na Lebanoni na Syria upande wa kaskazini, Ukingo wa Magharibi na Jordan upande wa mashariki, Ukanda wa Gaza na Misri upande wa kusini-magharibi, na Bahari ya Mediterranean upande wa magharibi. Israel pia ina pwani ndogo kwenye Bahari ya Shamu kwenye pointi yake ya kusini kabisa, na sehemu ya Bahari ya Chumvi inapatikana kando ya mipaka yake ya mashariki. Mji wake mkuu ni Yerusalemu, wakati Tel Aviv ni eneo kubwa la mijini na kituo cha kiuchumi cha nchi hiyo.
Israel מדינת ישראל (Kiebrania) دَوْلَةْ إِسْرَائِيل (Kiarabu) | |
---|---|
Wimbo wa taifa: "Hatikvah" | |
Mji mkuu na mkubwa | Jerusalem |
Lugha rasmi | Kiebrania |
Kabila (2025) | 73.5% Wayahudi 21.1% Waarabu 5.4% Wengine |
Serikali | Jamhuri ya Muungano wa Rais |
• Rais | Isaac Herzog |
• Waziri Mkuu | Benjamin Netanyahu |
Uhuru kutoka Uingereza | |
• Uhuru | 14 Mei 1948 |
Eneo | |
• Jumla | km2 20,770 km² |
• Maji (asilimia) | 2.71% |
Idadi ya watu | |
• Kadirio la 2025 | ▲ 10,009,800 |
• Msongamano | 454/km²/km2 |
PLT (PPP) | Kadirio la 2025 |
• Jumla | ▲ $565.878 bilioni (ya 47) |
• Kwa kila mtu | ▲ $55,847 |
PLT (Kawaida) | Kadirio la 2025 |
• Jumla | ▲ $550.905 bilioni |
• Kwa kila mtu | ▲ $54,370 |
HDI (2022) | 0.915 |
Sarafu | Shekel Mpya ya Israeli (₪) ILS |
Majira ya saa | UTCIST (UTC+2) |
Upande wa magari | Kulia |
Msimbo wa simu | +972 |
Jina la kikoa | .il |
Tanbihi: Eneo jumla la Israeli pamoja na Golan Heights na Jerusalem ya Mashariki ni 22,072 km² |
Historia
Nchi ya kisasa ilianzishwa tarehe 14 Mei 1948 lakini nyuma kuna historia ndefu, ambayo kwa sehemu muhimu inasimulia na Biblia kama kiini cha historia ya wokovu.
Mji mkuu umekuwa Yerusalemu tangu mwaka 1950 lakini nchi nyingi hazikubali kuwa hivyo kwa sababu hali yake kadiri ya Sheria ya kimataifa haieleweki.
Demografia
Takriban 74.9% za wakazi ni Wayahudi ambao wengi wao wanafuata dini ya Uyahudi, na 20.7 % ni Waarabu ambao wengi ni Waislamu (16%) lakini pia Wakristo (2% za raia wote: kati ya Wakristo hao karibu 80% ni Waarabu). Wahamiaji wengi wasiopata uraia ni Wakristo.
Lugha rasmi ni Kiebrania na Kiarabu. Lugha nyingine zinazotumika sana nyumbani ni Kirusi, Kifaransa na Kiamhari, mbali ya Kiingereza.
Tazama pia
Viungo vya nje
- (Kiingereza) (Kiarabu) na (Kiebrania) Tovuti ya serikali
- Israel blog Ilihifadhiwa 3 Novemba 2009 kwenye Wayback Machine.
Nchi na maeneo ya Asia |
Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iraq | Israel | Jamhuri ya China (Taiwan) | Japani | Kamboja | Kazakhstan | Kirgizia | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Laos | Lebanoni | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Saudia | Singapuri | Sri Lanka | Syria | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Turkmenistan | Uajemi | Ufilipino | Uhindi | Urusi1 | Uthai | Uturuki1 | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani |
1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi iko Asia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China. |
Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Israel kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. |