Mbwa-mwitu Dhahabu

Mbwa-mwitu dhahabu
Bweha mashariki (Canis anthus bea)
Bweha mashariki (Canis anthus bea)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mammalia (Wanyama wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao)
Oda: Carnivora (Wanyama mbua)
Nusuoda: Caniformia (Wanyama kama mbwa)
Familia: Canidae (Wanyama walio na mnasaba na mbwa)
Nusufamilia: Caninae
Jenasi: Canis
Linnaeus, 1758
Spishi: C. anthus
F. Cuvier, 1820
Ngazi za chini

Nususpishi 6:

Msambao wa mbwa-mwitu dhahabu
Msambao wa mbwa-mwitu dhahabu

Mbwa-mwitu dhahabu (pia bweha-dhahabu, bwea dhahabu, mbweha dhahabu na bweha-mbuga) ni mnyama wa jamii ya mbwa anayetokea Afrika ya Kaskazini na ya Mashariki. Zamani jina lake la kisayansi lilikuwa Canis aureus, lakini hivi karibuni wataalamu wamebaini kwamba nususpishi za Afrika ni tofauti na zile za Asia na Ulaya. Kwa hivyo nususpishi za Afrika zimepata jina jipya Canis anthus[1]. Hadi sasa bado huitwa bweha na watu wengi lakini yuko karibu zaidi na Mbwa-mwitu Habeshi na Mbwa-nyika (coyote) wa Amerika ya Kaskazini. Kwa hivyo tafadhali aitwe mbwa-mwitu.

Anapatikana Kenya na kaskazini kwa Tanzania (k.m. Hifadhi ya Serengeti) ambayo ni kusini kabisa ya uenezaji wake.

Mbwa-mwitu dhahabu hula wanyama wadogo hadi ukubwa wa swala, mizoga, wadudu na matunda. Makazi yake ni jangwa, mbuga na misitu myepesi. Anaishi kwa vikundi vidogo hasa dume na jike pamoja na watoto.

Kwa jumla kuna nususpishi 6 zinazo tambuliwa:

Tanbihi hariri

  1. Koepfli, K.-P.; Pollinger, J.; Godinho, R.; Robinson, J.; Lea, A.; Hendricks, S.; Schweizer, R. M.; Thalmann, O.; Silva, P.; Fan, Z.; Yurchenko, A. A.; Dobrynin, P.; Makunin, A.; Cahill, J. A.; Shapiro, B.; Álvares, F.; Brito, J. C.; Geffen, E.; Leonard, J. A.; Helgen, K. M.; Johnson, W. E.; O'Brien, S. J.; Van Valkenburgh, B.; Wayne, R. K. (2015-08-17). "Genome-wide Evidence Reveals that African and Eurasian Golden Jackals Are Distinct Species". Current Biology 25: 2158–65. PMID 26234211. doi:10.1016/j.cub.2015.06.060. 

Marejeo hariri

  • Sillero-Zubiri, C. (2009). Family Canidae (Dogs). (352-447). In: Wilson, D. E., Mittermeier, R. A., (Hrsg.). Handbook of the Mammals of the World. Volume 1: Carnivores. Lynx Edicions, 2009. ISBN 978-84-96553-49-1