Nyoka-maji (Grayia)

Nyoka-maji
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Reptilia (Wanyama wenye damu baridi na magamba ngozini)
Oda: Squamata (Mijusi, mijusi-nyungunyungu na nyoka)
Nusuoda: Serpentes (Nyoka)
Familia: Lamprophiidae (Nyoka walio na mnasaba na chata)
Fitzinger, 1843
Nusufamilia: Grayiinae (Nyoka wanaofanana na nyoka-maji)
Vidal, Delmas, David, Cruaud, Couloux & Hedges, 2007
Jenasi: Grayia
Günther, 1858
Ngazi za chini

Spishi 4:

Nyoka-maji wa jenasi Grayia ni nyoka wasio na sumu katika familia Lamprophiidae. Kuna nyoka-maji katika jenasi Lycodonomorphus wa familia hiyo hiyo pia, lakini nyoka hawa ni wafupi zaidi kwa kima cha 50%.

Nyoka hawa ni warefu kiasi. Spishi kubwa inaweza kufika m 2.5 lakini urefu wa wastani ni sm 70-150. Wana mkia mrefu (hadi 40% ya urefu wa jumla). Rangi yao ni hudhurungi hadi nyeusi na kuna mabaka meupe au kijivu mbavuni.

Spishi za Grayia huishi majini katika misitu ya mvua ya Afrika ya Kati na spishi mbili zinatokea Afrika ya Mashariki pia. Hula vyura na samaki wadogo.

Nyoka hawa hawana sumu na kwa hivyo wanaweza kukamatwa bila hatari licha ya urefu wao.

Spishi hariri

Marejeo hariri

  • Spawls, S., Howell, K., Drewes, R. & Ashe, J. (2002) A field guide to the Reptiles of East Africa. Academic Press, San Diego, CA, USA.

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mnyama fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Nyoka-maji (Grayia) kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.