Yesu kushushwa
(Elekezwa kutoka Pietà)
Yesu kushushwa kutoka msalabani mara baada ya kufa na kupakatwa na mama yake, Bikira Maria, ni tukio lililofikiriwa na wafuasi wake wengi na kuchorwa au kuchongwa na wasanii mbalimbali kwa ufanisi mkubwa.
Maarufu zaidi ni sanamu ambayo ilichongwa katika marumaru na Michelangelo Buonarroti na inatunzwa katika basilika la Mtume Petro huko Vatikani.
Aina hiyo ya sanaa inaitwa kwa kawaida "Pietà", neno la Kiitalia linalomaanisha huruma.
Tanbihi hariri
Marejeo hariri
- Forsyth, William F. (1995). The Pietà in French late Gothic sculpture: regional variations. New York: The Metropolitan Museum of Art. ISBN 0-87099-681-9.
Viungo vya nje hariri
Wikimedia Commons ina media kuhusu: