Sanamu ni kazi ya sanaa ambayo inatofautiana na picha au mchoro kwa sababu inaonyesha mtu au kitu si kwa urefu na upana, bali pia kwa unene.

Mtu akifikiri, kazi ya Rodin, 1902 hivi, Bronzi, Copenhagen, Denmark
Leshan Giant Buddha, 803 hivi, iliyochongwa katika mlima, Leshan, China
Uwiano wa uasilia, VUDA Park, Visakhapatnam, India
Sanamu ya moai, Kisiwa cha Pasaka, Chile

Inaweza kutengenezwa kwa kuchonga au kwa njia nyingine (k.mf. kumimina kiowevu katika muundo uliokusudiwa).

Historia hariri

Sanamu zilitengenezwa tangu zamani za historia ya awali (walau miaka 30,000 hivi iliyopita) na katika utamaduni mbalimbali wa dunia nzima. Ile ndefu zaidi ni sanamu ya Buddha inayopatikana China ikiwa na urefu wa mita 128.

Mara nyingi sanamu inaagizwa kama kumbukumbu ya tukio fulani au mtu maarufu na inawekwa mahali pa hadhara.

Katika dini hariri

Dini mbalimbali, hasa Uyahudi na Uislamu, zimekataza sanamu na picha zote.

Katika Ukristo suala lilijadiliwa kwa nguvu zote hasa katika karne ya 7 na ya 8 likamalizika katika mtaguso wa pili wa Nisea. Hata hivyo, baadaye lilizuka tena na tena, hivi kwamba msimamo wa madhehebu ni tofauti sana.

Picha hariri

Tanbihi hariri

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii kuhusu mambo ya utamaduni bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Sanamu kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.