Radio France Internationale


Radio France Internationale (RFI; Redio ya Dunia ya Ufaransa) imeasisiwa kwa jina hili na serikali ya Ufaransa katika 1975 kama sehemu ya Radio France. Ilikuwa imefanya kazi tangu 1931 kwa majina mbalimbali. Katika 1986 Ubunge wa Ufaransa ulibadilisha sheria ili kuruhusu RFI ifanye kazi bila udhibiti wa Radio France.

Nembo la RFI
Nembo la RFI
Kutoka mji Paris
Nchi Ufaransa
Eneo la utangazaji ulimwenguni kote
Kituo kilianzishwa mwaka Januari 1975
Mwenye kituo serikali ya Ufaransa
Programu zinazotolewa idhaa za redio kwa lugha za dunia
Tovuti rfi.fr
RFI kwe kiswahili

RFI inafanya kazi chini ya himaya ya Waziri wa Ufaransa wa Mambo ya Nchi za Nje na inapata pesa kutoka kwa bajeti yake. Inatangaza kwa Kifaransa hasa lakini kwe Kiingereza, Kiswahili, Kihausa, Kihispania, Kireno, Kiromania, Kirusi, Kiajemi, Kichina, Kivietnam na Kikhmer pia. Inamiliki pia Redio w:Monte Carlo Doualiya inayotayarisha vipindi kwa Kiarabu katika Paris na kuvitangazia hadhira katika Afrika ya Kaskazini na Mashariki ya Kati kutoka transmita katika Kupro.

Marejeo

  Makala hii kuhusu vituo vya redio bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Radio France Internationale kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.