Sabah Al-Ahmad Al-Jaber Al-Sabah

Sabah al-Ahmad al-Jaber al-Sabah (kwa Kiarabu: الشيخ صباح الأحمد الجابر الصباح‎; 16 Juni 1929 - 29 Septemba 2020) alikuwa Emir wa Kuwait na Kamanda wa Vikosi vya Jeshi vya Kuwait. Aliapishwa tarehe 29 Januari 2006 baada ya kuthibitishwa na Bunge na alihudumu hadi kifo chake tarehe 29 Septemba 2020.

Alikuwa mtoto wa nne wa Sheikh Ahmad Al-Jaber Al-Sabah.