Shushani (kwa kwa Kigiriki τά Σοῦσα Susa, leo شوش Shush kwa Kiajemi) [1] ni mji wa kale kusini mwa Iran.[2]

Kibao kinachoonyesha kuharibiwa kwa Susa na Ashurbanipal mwaka wa 647 KK

Uko upande wa kusini mwa Milima ya Zagros, takriban kilomita 250 mashariki mwa Mto Hidekeli na iko kati ya mito Karkheh na Dez. [2]

Ni mmoja kati ya miji ya kale sana. Kuanzia milenia ya tatu hadi milenia ya kwanza kabla ya Kristo Shushani ulikuwa mji mkuu wa milki ya Elamu.

Katika Karne ya 6 KK ulikuwa sehemu ya milki ya Waakhameni (Uajemi). Hapo ilikuwa mmoja kati ya miji mikuu minne ya wafalme wa Uajemi. Unatajwa vile katika Kitabu cha Esta cha Biblia.

Baada ya uvamizi wa Aleksanda Mkuu, Shushani iliona arusi iliyoamriwa ya maafisa wakuu Wagiriki 80 na wanawake Waajemi.

Chini ya watawala Waparthi na Wasasani, Shushani haukuwa mji mkuu tena lakini iliendelea kuwa kitovu cha biashara na uchumi.

Hata baada ya uvamizi wa Waarabu walioleta utawala wa Kiislamu mji ulikuwa muhimu. Lakini wakati wa uvamizi wa Wamongolia kwenye mwaka 1218 mji uliharibika na wakazi wengi kuuawa. Leo hii mji unaitwa Shush ukiwa na wakazi 64,960.

Marejeo hariri

  1. Morwood, James; Taylor, John, wahariri (2002). Pocket Oxford Classical Greek Dictionary (toleo la First). Oxford University Press. uk. 364. ISBN 978-0-19-860512-6. 
  2. 2.0 2.1 Lendering, Jona. "Susa, capital of Elam". Iran Chamber Society. Iliwekwa mnamo 2011-11-27.