Sulpisi Pius (alifariki Bourges, leo nchini Ufaransa, 17 Januari 647) alikuwa askofu wa mji huo kuanzia mwaka 624, baada ya kuishi ikulu. Alijali kuliko yote huduma kwa maskini na alikamilisha kazi ya kuinjilisha wakazi wa jimbo lake kwa kuwavuta Wayahudi na Wapagani wa mwisho katika Ukristo[1].

Sanamu yenye masalia yake.

Tangu kale anaheshimiwa na Kanisa Katoliki na Kanisa la Kiorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake ni tarehe 17 Januari[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.