Tibesti ni safu ya milima nchini Chadi na pia Libya yenye milima mikubwa zaidi ya eneo lote la jangwa la Sahara. Asili yake ni ya kivolkeno.

Volkeno ya Emi Koussi katika safu ya Tibesti

Mlima wenye kimo kirefu ni Emi Koussi (m 3415), Kegueur Terbi (m 3376), Tarso Taro (m 3325) na Pic Tousside (m 3265) ambayo ni volkeno hai.

Sehemu za juu mlimani hupokea mvua kidogo kila mwaka, kiasi hadi sentimita 12, kinachowezesha kustawi kwa mimea na hata miti kadhaa. Kwa hiyo kuna wakazi wachache wa kudumu.

Zamani, kabla ya kuenea kwa Sahara, eneo lilikuwa na wanyamapori wengi, jinsi inavyoonekana katika michoro kwenye mapango yaliyokuwa makazi ya binadamu takriban miaka 5000 iliyopita (yaani mnamo 3000 KK).

Viungo vya nje hariri