Upofu wa mto

(Elekezwa kutoka Usubi (ugonjwa))

Upofu wa mto(ni) au usubi (pia inajulikana kama Onchocerciasis na Maradhi ya Robles), ni maradhi yasababishwayo na ambukizo la kinyoo wa kimelea Onchocerca volvulus.[1]

Upofu wa mto
Mwainisho na taarifa za nje
SpecialtyInfectious diseases, tropical medicine Edit this on Wikidata
ICD-10B73.
ICD-9125.3
DiseasesDB9218
eMedicinemed/1667 oph/709
MeSHD009855

Dalili ni pamoja na mwasho mkali, manundu chini ya ngozi, na upofu. Maradhi hayo ni sababu ya pili baada ya vikope kumfanya mtu kuwa kipofu kutokana na ambukizo.[2]

Chanzo na uaguaji hariri

Mwaka wa 1915 daktari Rodolfo Robles aligundua kwa mara ya kwanza uhusiano baina ya kinyoo na maradhi ya macho.[3]

Kinyoo cha kimelea anasambazwa na maumo ya usubi weusi wa spishi fulani za jenasi Simulium.[1] Kwa kawaida maumo mengi yanahitajika kabla ya ambukizo kuumiza.[4]

Usubi hao huishi karibu na mito: ndiyo sababu ya jina “upofu wa mto”.[2]

Mara tu vinyoo wameshaingia mwilini wanaunda kiluwiluwi ambao wanatembea hadi nje, juu ya ngozi ambapo wanaweza kumwambukiza nzi aliyekuja kuuma binadamu husika.[1]

Utambuzi hariri

Kuna namna kadhaa za kufanyia uanguaji nazo ni pamoja na: kutia tishu ya ngozi iliyokatwa ndani ya mchanganyiko wa maji yenye asilimia 0.9 ya chumvi ukasubiri kiluwiluwi kutokea, kuchunguza jicho kwa dalili za kiluwiluwi, na kuchunguza manundu yaliyo chini ya ngozi kugundua vinyoo wazima.

Kinga na tiba hariri

Hakuna dawa ya chanjo dhidi ya maradhi hayo. [1] Ugangakinga ni kujiepusha na kuumwa na nzi.[5]

Namna za kusaidia kujiepusha ni pamoja na dawa za kinga dhidi ya vidudu na mavazi yanayofaa. [5] Taratibu zingine ni zile za kupunguza idadi ya nzi kwa kupulizia dawa za kuua wadudu.[1]

Bidii zenye kufutilia kabisa maradhi hayo katika dunia nzima kwa kuwatibu mara mbili kwa mwaka watu walio pamoja katika makundi zinatendeka sehemu kadhaa za dunia.[1]

Matibabu ya wale walioambukizwa ni kuwapa dawa ya ivermectin kila baada ya miezi sita au miezi kumi na mbili.[1][6] Matibabu hayo huua kiluwiluwi lakini hayawaui vinyoo wazima.[7]

Dawa ile ya doxycycline ambayo huua bakteria waitwao Wolbachia nayo ikihusika na [[endosymbiont] inaonekana kudhoofisha vinyoo ikapendekezwa vilevile.[7] Upasuaji wenye kuondoa manundu vilevile unatendeka. [6]

Takwimu hariri

Takriban watu milioni 17 hadi 25 wanaambukizwa upofu wa mto, huku takriban milioni 0.8 wamekosa kiasi fulani cha uwezo wa kuona.[4][7]

Maambukizo kwa wingi hutokea barani Afrika kusini kwa Sahara, ingawa wengine wanaoishi Yemen pamoja na sehemu za upweke za Amerika ya Kati na Amerika ya Kusini wameambukizwa.[1]

Maradhi hayo yanaelezwa kuwa maradhi ya nchi za joto yasiyoangaliwa na Shirika la Afya Duniani. [8]

Marejeo hariri

  1. 1.0 1.1 1.2 1.3 1.4 1.5 1.6 1.7 "Onchocerciasis Fact sheet N°374". World Health Oragnization. March 2014. Iliwekwa mnamo 20 March 2014.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  2. 2.0 2.1 "Onchocerciasis (also known as River Blindness)". Parasites. CDC. May 21, 2013. Iliwekwa mnamo 20 March 2014.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  3. Lok, James B.; Walker, Edward D.; Scoles, Glen A. (2004). "9. Filariasis". Katika Eldridge, Bruce F.; Edman, John D.; Edman, J. Medical entomology (toleo la Revised). Dordrecht: Kluwer Academic. uk. 301. ISBN 9781402017940. 
  4. 4.0 4.1 "Parasites – Onchocerciasis (also known as River Blindness) Epidemiology & Risk Factors". CDC. May 21, 2013. Iliwekwa mnamo 20 March 2014.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  5. 5.0 5.1 "Onchocerciasis (also known as River Blindness) Prevention & Control". Parasites. CDC. May 21, 2013. Iliwekwa mnamo 20 March 2014.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  6. 6.0 6.1 Murray, Patrick (2013). Medical microbiology (toleo la 7th). Philadelphia: Elsevier Saunders. uk. 792. ISBN 9780323086929. 
  7. 7.0 7.1 7.2 Brunette, Gary W. (2011). CDC Health Information for International Travel 2012 : The Yellow Book. Oxford University Press. uk. 258. ISBN 9780199830367. 
  8. Reddy M, Gill SS, Kalkar SR, Wu W, Anderson PJ, Rochon PA (October 2007). "Oral drug therapy for multiple neglected tropical diseases: a systematic review". JAMA 298 (16): 1911–24. PMID 17954542. doi:10.1001/jama.298.16.1911.  Check date values in: |date= (help)
  Makala hii kuhusu mambo ya tiba bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Upofu wa mto kama sababu yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.