Alpaka

(Elekezwa kutoka Vicugna)
Alpaka
Alpaka asiyenyoleka akila (Vicugna pacos)
Alpaka asiyenyoleka akila
(Vicugna pacos)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Mamalia (Wanyama wenye viwele wanaonyonyesha wadogo wao)
Oda: Artiodactyla (Wanyama wenye vidole viwili au vinne mguuni)
Nusuoda: Tylopoda (Wanyama wenye miguu inayovimba)
Familia: Camelidae (Wanyama walio na mnasaba na ngamia)
J. E. Gray, 1821
Jenasi: Vicugna (Alpaka na vikunya)
Lesson, 1842
Spishi: V. pacos (Alpaka)
(Linnaeus, 1758)
Msambao wa alpaka
Msambao wa alpaka

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru

Alpaka ni mnyama wa kufugwa wa spishi Vicugna pacos katika familia Camelidae, anayeishi Amerika Kusini. Alpaka anafanana na lama mdogo, lakini ameainishwa katika jenasi tofauti. Kuna nususpishi mbili za alpaka; alpaka suri na alpaka huacaya.

Maelezo hariri

 
Uso wa alpaka kwa karibu

Kwa kawaida, alpaka mzima ana kimo cha sm 81–99 mabegani, na uzito wa kilo 48–84.

Alpaka hutunzwa kwa makundi na hulishwa katika nyanda za juu za milima ya Andes katika upande wa kusini wa Peru, kaskazini ya Bolivia, Ekuador, na kaskazini ya Chile, ambako wanaishi mita 3,500–5,000 juu ya usawa wa bahari, mwaka wote.[1] Alpaka ni wadogo kiasi kuliko lama, na tofauti na lama, hawakufugwa kuwa wanyama wa mizigo, badala yake walifugwa mahususi kwa ajili ya manyoya yao. Manyoya ya alpaka hutumiwa kutengeneza vitu vifumwavyo, mithili ya sufu. Vitu hivyo ni pamoja na mablanketi, sweta, kofia, glavu na nguo nyingine katika Amerika Kusini, na sweta, soksi, koti na matandiko katika sehemu nyingine duniani. Fumwele za manyoya yao zinapatikana katika zaidi ya rangi 52, kama zinavyoainishwa Peru.

Katika biashara ya vitambaa, maana ya msingi ya "alpaca" ni nywele za alpaka wa Peru lakini, kwa upana zaidi, "alpaca" inamaanisha mtindo wa vitambaa vilivyotengenezwa awali kutoka nywele za alpaka, ambavyo sasa vinatengenezwa mara nyingi kwa fumwele zinazofanana na nywele za alpaka, kama sufu za ubora sana.

Marejeo hariri

  1. Harvesting of textile animal fibres. UN Food and Agriculture Organization.
 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:

Ili kupata maelezo kuhusu masanduku ya uanapwa ya spishi angalia: Wikipedia:WikiProject Mammals/Article templates/doc.