Ekuador

ni nchi kwenye pwani ya magharibi ya Amerika Kusini

Ekuador (kwa Kiswahili pia: Ekwado) ni nchi kwenye pwani ya magharibi ya Amerika Kusini.

Ekuador


Ramani ya Ekuador

Jina la nchi kwa Kihispania (Ecuador) lamaanisha "ikweta", na sababu ni kwamba imekatwa nayo.

Imepakana na Kolombia, Peru na Bahari ya Pasifiki.

Funguvisiwa la Galapagos (Archipiélago de Colón) ni sehemu ya Ekuador ikiwa na umbali wa karibu kilomita 1,000 kutoka bara.

Mji mkuu ni Quito, lakini mji mkubwa zaidi ni Guayaquil.

Watu hariri

Wananchi wengi (71%) wana mchanganyiko wa damu ya Kizungu na ya Kiindio. Wenye asili ya Afrika ni 7.2%, Waindio ni 7%, na Wazungu ni 6.1%.

Ekuador ilikuwa koloni la Hispania, hivyo lugha ya wakazi wengi na lugha rasmi imekuwa Kihispania hadi leo. Lakini kuna Waindio wengi, hasa katika milima ya Andes, wanaoendelea kutumia lugha zao.

Asilimia 91.95 wana dini, na kati yao 80.44% ni Wakatoliki ma 11.3% Waprotestanti.

Tazama pia hariri

Viungo vya nje hariri

 
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
Nchi na maeneo ya Amerika Kusini

Argentina | Bolivia | Brazil | Chile | Ekuador | Guyana | Guyani ya Kifaransa | Kolombia | Paraguay | Peru | Surinam | Uruguay | Venezuela

  Makala hii kuhusu maeneo ya Amerika Kusini bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Ekuador kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.