Kiongozi

(Elekezwa kutoka Watawala)

Kiongozi ni mtu ambaye huongoza kikundi cha watu[1]. Mara nyingi kiongozi hupewa heshima ya juu katika jamii, kikundi cha watu au katika familia ambapo huheshimiwa na watu wote katika eneo husika analolisimamia kiongozi kwa ajili ya kuwaongoza watu.

Kiongozi wa Tanzania,J.P. Magufuli

Kiongozi katika jamii hariri

Katika nchi nyingi duniani kiongozi hupatikana kwa wananchi kupiga kura ambapo watu mbalimbali wanaogombea uongozi hupigwa kura kwa ajili ya kuwa kiongozi katika jamii au kikundi cha watu hupatikana[2].

Mara nyingine kiongozi huchaguliwa kwa kuteuliwa na mtu mmoja pasipo kupigwa kura.

Pia katika jamii nyingine kiongozi hupatikana kwa kurithi, ambapo mrithi huwa kiongozi kwa kurithi uongozi kutoka kwa kiongozi aliyefariki na kuachia madaraka.

Kiongozi katika familia hariri

Kiongozi katika familia huwa ni mtu aliye na umri mkubwa katika familia husika, ambapo viongozi huwa ni baba na mama. Katika familia nyingi baba ndio huwa kiongozi mkubwa akifuatiwa na mama.

Pia familia huweza kuwa na kiongozi wa ukoo ambapo bibi na babu huwa viongozi wa juu katika ukoo.

Kiongozi katika Biblia hariri

Katika Biblia kiongozi ni mtu ambaye humwakilisha Mungu katika kuongoza watu wake hapa duniani[3]. Hivyo anapaswa kukumbuka kwamba ameshirikishwa mamlaka ya juu na kwamba atapaswa kuhukumiwa kwa namna alivyoitumia.

Yesu alisema kwa kawaida watawala hutumia mabavu na hata hivyo hupenda kuitwa wafadhili.

Marejeo hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya utamaduni bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kiongozi kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.