Winnie Madikizela-Mandela

(Elekezwa kutoka Winnie Mandela)

Winnie Madikizela-Mandela (jina la kuzaliwa: Nomzamo Winifred Zanyiwe Madikizela; 26 Septemba 1936 - 2 Aprili 2018[1]) alikuwa mwanasiasa wa Afrika Kusini. Alijulikana kimataifa kama mpinzani wa siasa ya ubaguzi ya apartheid na mke wa Nelson Mandela.

Winnie Madikizela-Mandela

Baada ya mwisho wa apartheid alichukua nafasi za uongozi serikalini na katika chama cha ANC lakini alipaswa kujiuzulu baada ya mashtaka dhidi yake kupatikana.

Alikuwa maarufu kama mpiganaji wa haki wa watu weusi wa nchi yake. Wafuasi wake walimwita 'Mama wa Taifa'. Lakini alihusishwa pia katika mauaji wakati wa mapambano dhidi ya apartheid, hususani baada ya kukumbana na mashtaka mbalimbali kama vile, kukiukwa kwa haki za binadamu kama vile kumtesa na hatimaye kuuawa kwa mtoto wa miaka 14, Stompie Moeketsi mwaka 1989.[2]

Baadaye alihusishwa na udanganyifu na wizi. Kwa hiyo kumbukumbu yake ni ya mchanganyiko kama shujaa wa kupigania uhuru na mtu mwenye kasoro nyingi.[3]

Miaka ya awali, elimu hariri

Jina lake la asili la Kixhosa ni Nomzamo linalomaanisha „Anayejaribu“. Alizaliwa katika kijiji cha Mbogoweni, sehemu ya Bizana katika Mkoa wa Pondo ambayo sasa ni mkoa wa Eastern Cape huko Afrika Kusini. Baadaye alipokea ajira na kuishi katika sehemu mbalimbali kama Bantustan ya Transkei, Banzana, Shawbury na Johannesburg .

Alikuwa mtoto wa nne kati ya nane waliokuwa saba wa kike na mmoja wa kiume. Wazazi wake Columbus na Getrude walikuwa walimu. Mama aliaga dunia wakati Winnie alikuwa na miaka 8 na watoto waligawiwa kati ya ndugu wa wazazi.

Winnie-Nomzamo alisoma elimu ya sekondari huko Bizana akaendelea kusoma ustawi wa jamii mjini Johannesburg alipopewa stashahada yake 1956 akapata ajira katika huduma za jamii. Miaka ya baadaye aliongeza shahada ya awali (B.A.) katika somo la mahusiano ya kimataifa kwenye Chuo Kikuu cha Witwatersrand.

Ndoa na familia hariri

Alipofanya kazi ya huduma za jamii alikutana na mwanasheria na mwanaharakati wa kupinga ubaguzi wa rangi, Nelson Mandela, mwaka wa 1957. Walifunga ndoa mwaka wa 1958 na kujaliwa kupata binti wawili, Zenani (aliyezaliwa mwaka wa 1959) na Zindzi (aliyezaliwa mwaka wa 1960). Mumewe alikamatwa na serikali ya apartheid mwaka 1962 akaendelea kukaa gerezani hadi 1990. Katika muda huu mrefu Winni Mandela alijihusisha zaidi na zaidi na upinzani wa siasa ya ubaguzi wa rangi. Wakati mumewe alitoka gerezani ndoa ilikuwa matatani; walitengana rasmi mwaka 1992 hadi kumaliza talaka kisheria mwaka 1996.

Upinzani dhidi ya sera ya ubaguzi ya apartheid hariri

Aliibuka kama mpinzani muhimu wa siasa ya ubaguzi wa rangi iliyoweka mamlaka yote katika mikono ya watu weupe nchini Afrika Kusini. Kwa jitihada zake aliwekwa mara kadhaa gerezani au alizuliwa mwendo huru nje ya mji au mtaa fulani akipaswa kukaa kwa miaka kadhaa Brandfort katika eneo la Orange Free State. Mara chache tu aliruhusiwa kumtembelea mumewe katika gereza la Robben Island.

Katika miaka ya 1980 na miaka ya 1990, alivuta hisia za taifa na mataifa kwa ujumla, na alikuwa akifanyiwa mahojiano na waandishi wa habari wa kitaifa na kimataifa. Chama cha ANC kilichokuwa marufuku ndani ya Afrika Kusini alimtumia kama uso wa upinzani dhidi ya apartheid mbele ya umma wa kimataifa. Rais Thabo Mbeki alitaja nafasi hii katika barua ya mwaka 2008: „Katika muktadha wa mapambano ya kimataifa kwa ajili ya uhuru wa wafungwa wa kisiasa katika nchi yetu, harakati yetu ilichukua uamuzi wa kimakusudi kutumia jina la Nelson Mandela kama kielelezo cha wafungwa hawa. Hivyo tulitumia pia wasifu wake wa kibinafsi wa kisiasa, pamoja na mateso ya mkewe wa awali, Winnie Mandela, kuonyesha dunia na jamii ya Afrika Kusini ukatili wa mfumo wa ubaguzi wa rangi.“[4]

Kushtakiwa kwa unyanyasaji na mauaji hariri

Heshima yake ilishuka, kutokana na kile ambacho wengi wanaamini kua kiu ya damu. Mfano halisi wa hali hii ni hotuba yake aliyoitoa katika eneola Munsieville katika siku ya tarehe 13/04/1985. ambapo alikubali na kuaisha adhabu ya kuua watu kwa kuwavalisha matairi na kuweka mafuta ya Petrol na kisha kuwasha moto, katika harakati za kumaliza na kutokomeza mfumo wa Apartheid. Alisema kuwa, kwa kutumia viberiti vetu, na cheni zetu tutabadilisha nchi yetu.[5]

Mambo zaidi yaliyoshusha heshima yake,ni mashataka aliyoshtakiwa na mlinzi wake wa binafsi,Jerry Richardson, kuwa Winnie Madikezela Mandela ameagiza kukamatwa na kuuliwa tarehe 29/12/1989.Richard alimteka mtotowa miaka14, aiyeitwa James Seipei pia najulikana kama Stompie Moeketsi,na watoto wengine watatu, kutoka katika nyumba ya Waziri mchungaji Paul Verryn.Mrs Mandela alidai kuwa aliwachukua wototo hao na kuwapeleka katika nyumba yeke,kutokana na kuhisi kuwa Mchungaji huyo al ikuwa akiwanyanyasa kijinsia watoto hao.Watoto hao wanne,walipigwa sana iliwakubali kuwa walikuwa wakifanya mapenzi na mchungaji huyo. Pia Saipei alikuwa akidaiwa kuwa alikuwa mpelelezi. Mwili wa Saipei ulikutwa katika eneo la wazi ukiwa na vidodo vya kuchomwa tarehe 06/01/1990.[6]

Mwaka 1991 alikamatwa na kushtakiwa kwa makosa ya kuteka nyara na kuwa nyongeza katika mateso yaliyosababisha kifo cha Saipei. Kifungo chake cha miaka sita kilipunguzwa na kuwa kulipa faini baada ya kutokana na kukata rufaa

Kabla ya Mfumo wa ubaguzi / Apartheid hariri

Wakati wa mabadiliko ya Afrika ya kusini kuwa serikali ya Kidemokrasia, Winie alikuwa kidogo anawapendelea wazungu kuliko mume wake.Pamoja na kuwa na mume wake wakati akiachiwa huru mwakan1990.Miaka 38, ya ndoa ilimalizika walipaochana mwezi wa nne mwaka1992,baada ya kugundulika kuwa alikuwa sio mwaminifu kwa kipindi ambacho Mandela alipokuwa gerezani.Wawili hao walitalikiana mwezi wa tatu mwaka 1996.lakini alikuwa tayari kashapata jina la pili la Madikizela-Mandela. Alichaguliwa kuwa waziri wa sanaa,utamaduni, Sayansi na tekinolojia kama madaraka yake ya kwanza katika seriakali baada ya sera ya ubaguzi nchi humo yaani Apartheid.mwezi wa tano mwaka 1994,lakini alinyang'anywa wadhifa huo miezikumi na moja baadae baadaya kushutumiwa kwa kula rushwa.[7] Alibakia maarufu kwa wnachama wengi wa chamacha ANC, na mwezi wa kumi na mbili mwaka1993,alichaguliwa kugombea nafasi ya uraisi kwa tiketi ya chama ca ANC, chamacha wanawake.japokuwa alijivua wadhifa huo na kuwa makamu mwenyekiti wa Raisi wa chama hicho, katika harakati kwenye mkutanowa Mafikeng mwezi wa kumi na mbili mwaka 1997. Mwaka 1997,alitokezakatika baraza laUkweli na Mapatani.Mchungai Desmond Tutu, alitambua umuhimu wake na nafasi yake katika harakati za kupigania uhuru na usawa lakini alimwomba akubali makosa yake na aweze kuomba msamaha.Katika kujibu alisema na kukubaki kuwa mambo yalikwenda vibaya sana.

Mashtaka ya udanganyifu hariri

Tarehe 24/04/2003, alikutwa na hatia ya mashtaka 43 ya udanganyifu, 25 ya wizi, na msaidizi wake Addy Moolman, alishtakiwa kwa makosa 58 ya udanganyifu, 25 ya wizi. Wote wawili walikana mashtaka yanayotokana na fedha zilizopotea kutokana na maombi ya mkopo na gharama za mazishi,maombi ambayo waombwai hawayapata licha ya fedha kutolewa. Medikizela-Mandela alihukumiwa kifungo cha miaka mitano jela. .[8] Muda mfupi baada ya kuhukumiwa alistaafu nafasi zote alizokuwa nazo katika chama cha ANC cha wanawake.[9] Mwishoni mwa mwaka 2003, rafiki yake wakaribu, Hazel Crane aliuwawa.Crane hapo mwazo alitaka kununua nyumba ya Madikizela-Mandela. .[10] Mwezi wa saba mwaka 200,jajo wa mahakama kuu ya Pretoria alisemakuwa, makosa hayawezi kufanywa ili kumfaidisha mtu. Jaji huyo alimfutia mashtaka ya wizi na kuacha na mshtaka ya udanganyifu na hivyo kuanya kifungo chake kiwe cha miaka mitatu na miezi sita.[11]

Kunyimwa visa ya kuingia Canada hariri

Mwezi wa sita mwaka 2007, ubalozi wa Kanada nchini Afrika ya Kusini, ilikataa kumpa viza Winnie Mandela ya kusafiri hadi Toronto, Kanada ambapo alikuwa amepangiwa kushiriki katika tamasha la harambee lilopangwa na kituocha sanaa cha MusicNoir, ambacho kilijumuisha kuoneshwa kwa mara ya kwanza kwa tamthiliya ya The Passion of Winnie iliyokuwa imeigizwa kuendana na maisha yake. .[12]

Kurudi katika siasa hariri

Wakati chama cha ANC,kilipotangaza uchaguzi wa bodi ya uchaguzi ya taifa tarehe 21/12/2007.Mandela alishika nafasi ya kwanza kwa kuwa na kura 2845.[13][14]

Msamaha kwa wahanga wa maandamano hariri

Mandela aliyapinga mandamano yenye fujo ya kuanzia mwezi wa tano hadi mwezi wa sita mwaka 2008,yaliyoanza katika jiji la Johannesburg na kuenea katika nchi nzima na kuilaumu serikali kw kutokuwa na kushindwa kutoa huduma ya makazi kwa waathirika wa maandamano.[15] Pia aliomba msamaha kwa waathirika walipata matatio kutokana na maandamano.riots[16]. Halikadhalika alikwenda kuwatembelea waathirika hao katika mji wa Alexandra.]].[17] Pia alijitolea nyumba yake kwa ajili ya wahamiaji kutoka nci ya jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.[18] Alionya kuwa wapanda maandamano wangeweza kuvamia katika mfumo wa reli ya Gauteng.

Uchaguzi mkuu wa mwaka 2009 hariri

Mandela alishika nafasi ya tano katia uchaguzi ANC,kwa ajili ya uchaguzi wa mwaka 2009, waliokuwa mbele yakewalikuwa ni pamoja na Raisi wa sasa wa Afrika ya Kusini Jacob Zuma aliyekuwa raisi wa Afrika ya kusini Kgalema Motlante, Makamu wa raisi wa Afrika Kusini Baleka Mbete na Waziri wa fedha Trevo Manuel. Makala katika gazetila the Observer, lilisema kuwa, suala la Winnie kupata nafasi ya juu katika chaguzi hiyoinaonesha kuwa,chama chake kina imani nae sana na pia yeye ni hazina katika chama hicho hususani kwa watu masikini.[19]

Muonekano wake katika filamu na televisheni hariri

Tina Lifford anmwelezea Mandela, mwaka 1997, katika tamthilia ya mandela and De Klerk,[20] Sophia Okedo anamwelezea Mandela katika tamthiliya katika kituo cha televishei cha BBC.[21] Jennifer Hudson atacheza nafasi ya mama Mandela katika mchezo unaofuatia na utakaoazwa kurekodiwa mwaka 2010. Jennifer Hudson amekuwa akicheza nafasi ya Mandela katika filamu ya inayoitwa "Winnie" itakayoongozwa na Darrel J. Roodt. Andre Pieterse, Roodt na Paul L.Johnson inayoegemea katika mwongozo wa Anne Marie du Preez Bezdrob inayohusu historia ya maisha yake "Winnie Mandela: A life [22] Umoja wa wafanyakazi wa Afrika ya kusini,wamepinga mpango huu, na kueleza kuwa watafungua mashtaka kupinga filamu hiyoiwapo mpangilio wa waigizaji hautabadishwa.[23]

Marejeo hariri

  1. Winnie Madikizela has died. heraldlive.co.za ya 2 Aprili 2018, iliangaliwa 3 Aprili 2018
  2. Winnie says evidence against her is 'ludicrous'. BBC News (1997-12-04). Iliwekwa mnamo 2009-08-25.
  3. Winni Mandela, mother then mugger of new South Africa, huduma ya Reuters, iliangaliwa 3 Aprili 2018
  4. “In the context of the global struggle for the release of political prisoners in our country, our movement took a deliberate decision to profile Nelson Mandela as the representative personality of these prisoners, and therefore to use his personal political biography, including the persecution of his then wife, Winnie Mandela, dramatically to present to the world and the South African community the brutality of the apartheid system“ Thabo Mbeki's letter to Jacob Zuma, date=2008-10-31
  5. "Row over 'mother of the nation' Winnie Mandela", The Guardian, 27 Januari 1989. 
  6. "Winnie Mandela Aide Guilty of Murder", The New York Times, 26 Mei 1990. 
  7. Fred Bridgland (2003-04-26). Winnie Mandela's fall from grace. The Scotsman. Iliwekwa mnamo 2009-03-24.
  8. "ANC: We won't dump Winnie", Sunday Times (South Africa), 27 Aprili 2003. 
  9. "Winnie Mandela resigns ANC posts", CNN, 25 Aprili 2003. 
  10. High society rocked by the shady past of one of its own. The Age (2004-12-24).
  11. "Winnie: No personal gain", News24, 7 Mei 2004. Retrieved on 2009-12-26. Archived from the original on 2007-09-30. 
  12. "Winnie Mandela denied entry to Canada for arts gala", CBC.ca, 2007-06-05. Retrieved on 2007-06-05. Archived from the original on 2007-06-07. 
  13. Newly-elected National Executive Committee Archived 25 Mei 2010 at the Wayback Machine.,ANC Website, Retrieved on 21 Desemba 2007
  14. Winnie Mandela tops ANC election list Archived 2 Oktoba 2008 at the Wayback Machine., The Times, 21 Desemba 2007, Retrieved on 21 Desemba 2007
  15. Winnie speaks out on SA's issues
  16. Refugees flee South Africa attacks
  17. Winnie visits Alexandra. Jalada kutoka ya awali juu ya 2009-12-19. Iliwekwa mnamo 2009-12-26.
  18. Winnie adopts refugee family. Jalada kutoka ya awali juu ya 2008-05-30. Iliwekwa mnamo 2009-12-26.
  19. Winnie set for shock comeback to ANC politics
  20. http://www.imdb.com/title/tt0119607/fullcredits#cast
  21. Dowell, Ben. "BBC commissions Winnie Mandela drama", guardian.co.uk, Guardian News and Media, 11 Machi 2009. Retrieved on 11 Machi 2009. 
  22. Jennifer Hudson to star in 'Winnie'
  23. "South African actors 'want Hudson out of Mandela film'", American Free Press, 7 Desemba 2009. Retrieved on 8 Desemba 2009. 

Viungo vya nje hariri